• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC amtaka Mkandarasi kutoa maelezo

Posted on: June 13th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Ally Hapi ametoa saa 48 kwa mkandarasi anayejenga Uwanja wa Ndege Musoma kufika ofisini kwake kutoa maelezo kwa nini maelekezo aliyoyatoa kuhusiana na ujenzi wa uwanja huo hayajatekelezwa.

Mheshiwa Hapi ametoa maagizo hayo leo katika kikao cha wakandarasi wanaotekeleza miradi yao katika Mkoa wa Mara kilichofanyika katika Ukumbi wa Uwekezaji uliopo katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

“Ninatoa saa 48 huyo mkandarasi afike kutoa maelezo kwa nini maelekezo niliyoyatoa mwezi Machi, 2022 hayajafanyiwa kazi mpaka sasa na mradi bado upo nyuma sana katika utekelezaji wake” alisema Mheshimiwa Hapi.  

Mheshimiwa Hapi amefikia hatua hiyo baada ya mwakilishi wa Mkandarasi huyo Beijing Construction Engineering Group (BCEG) kushindwa kutoa maelezo kwa nini maagizo ya Mkuu wa Mkoa aiyoyatoa hayajatekelezwa.

Awali Mkuu wa Mkoa wa Mara akiwa ameambatana na wajumbe wa Bodi ya Barabara ya Mkoa wa Mara walitembelea mradi huo tarehe 1 Machi, 2022 na kukagua maendeleo ya ujenzi pamoja na kupatiwa taarifa.

Akiwa katika mradi huo, Mkuu wa Mkoa aliwagiza mkandarasi kuhakikisha mradi huo unakamilika kwa mujibu wa mkataba tarehe 30 Desemba, 2022 ili ndege za abiria ziweze kuanza kutua katika uwanja huo.

Mheshimiwa Hapi alimwagiza mkandarasi kufunga taa na kufanyakazi kwa saa 24, kuongeza vifaa na watumishi katika utekelezaji wa mradi huo, hata hivyo maagizo hayo hayajatekelezwa na mwakilishi wa mkandarasi alisema haiwezekani mradi huo kukamilika kwa muda uliobakia.

Maelezo ya Meneja wa Wakala Barabara (TANROADS) ambao ndio wasimamizi wa mradi huo, kwa sasa mradi huo upo katika asilimia 18 wakati muda wa utekelezaji wa mradi umeshafika asilimia 52.

Aidha mkandarasi ameshalipwa malipo ya awali na kwa sasa hana madai ya malipo ambayo ameshayawasilisha kwa TANROADS.

Uwanja wa Ndege wa Musoma ni muhimu katika kukuza uchumi wa Mkoa wa Mara na kurahisisha safari za watalii wanaoingia Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, kukwama kwa ukamilishaji wa uwanja huu kunaathiri uchumi wa Mkoa na wananchi wa Mkoa wa Mara.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa