• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC amkaribisha Kamishna Jenerali wa Uhamiaji

Posted on: July 8th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo ofisini kwake amempokea na kuzungumza na Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala ambaye amefanya ziara ya kikazi katika Mkoa wa Mara.

Akizungumza baada ya kuwasili, Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala amempongeza Mhe. Mtambi kwa kuaminiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kuuongoza Mkoa wa Mara.

Kamishna Makakala ameeleza kuwa lengo la ziara yake katika Mkoa wa Mara ni kushughulikia maombi ya walowezi wa muda mrefu ambao walihamia kutoka nchi ya Kenya ambao wanadai vitambulisho vya uraia.

“Tunashughulikia vitambulisho hivyo ili tunapoelekea kwenye uchaguzi wale wanaostahili kupata vitambulisho hivyo wawe navyo ili iwasaidie katika kutumia haki yao ya kuchagua viongozi” amesema Dkt. Makakala.

Dkt. Makakala amesema ofisi yake inashughulikia changamoto za ofisi ya Kamanda wa Uhamiaji Mkoa wa Mara ikiwemo suala la upungufu wa watumishi na usafiri kwa maafisa wa uhamiaji.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi amemshukuru Kamishna Jenerali wa Uhamiaji kwa kufanya ziara katika Mkoa wa Mara na kumshukuru kwa ushirikiano wa ofisi ya Uhamiaji Mkoa wa Mara kwa viongozi wa Mkoa.

Mhe. Mtambi amesema Mkoa wa Mara una waloweze wengi ambao wamekuwa wakifuatilia kadi ya mpiga kura, namba ya utambulisho wa Taifa na vitambulisho vingine vya uraia na wamekuwa wakiwatumia wanasiasa kufuatilia vitambulisho hivyo.

Mhe. Mtambi amemuomba Dkt. Makakala asiondoke kabla ya kuonja nyama choma ya Mkoa wa Mara na kutokana na mifugo yake kufugwa kwenye mazingira mazuri na kujionea utamu na ubora wa nyama choma ya Mkoa wa Mara.

“Haya mazingira inaonekana Mungu aliyaandaa kwa ajili ya wanyama na ndio maana sehemu kubw aya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ipo Mkoa wa Mara bahati mbaya wanyama hawa hawauzwi sana Tanzania wanapelekwa nchi jirani kwa njia ya magendo” amesema Mhe. Mtambi.  

Katika ziara hiyo, Kamishna Jenerali wa Uhamiaji ameambatana na Maafisa mbalimbali kutoka Jeshi la Uhamiaji Makao Makuu na Ofisi ya Uhamiaji Mkoa wa Mara.  

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa