• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC Akataa gharama za mradi wa TEMESA MUSOMA

Posted on: November 5th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi leo tarehe 13 Oktoba 2021 amekataa gharama za mradi wa ujenzi wa jengo la kupumzikia abiria linalojengwa katika Kivuko cha Mwigobero katika Manispaa ya Musoma unaotekelezwa na Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA).

Akizungumza baada ya kukagua na kupokea taarifa za ujenzi wa mradi huo, Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa gharama zinazotarajiwa kutumika katika mradi huo ni kubwa na haziendani na mradi wenyewe.

“Haiwezekani mradi huu hapa ambao ukubwa wake ni sawa na darasa moja utumie shilingi milioni 86, mimi kama Mkuu wa Mkoa nemeukataa mpaka hapo nitakapopata maelezo ya kuridhisha kuhusu gharama hizi” alisema Mheshimiwa Hapi.

Hata hivyo Mheshimiwa Hapi ameipongeza TEMESA kwa kutekeleza kwa haraka maagizo yake aliyoyatoa mwezi Mei mwaka huu akiwa katika ziara kukagua miradi ya maendeleo katika Wilaya ya Musoma.

“Kutekeleza maagizo yangu ni jambo moja, kutekeleza kwa ukweli, uaminifu na uadilifu ni jambo jingine, sikubaliani na gharama hizi” alisema Mheshimiwa Hapi.

Amemtaka Kaimu Meneja wa TEMESA kuwasilisha michoro na makadirio haliso ya gharama za ujenzi huo ofisini kwake ili kujiridhisha na gharama hizo za mradi.

Awali, akitoa taarifa kwa Mkuu wa Mkoa, Kaimu Meneja wa TEMESA Mkoa wa Mara Bwana Vitalis Bilauri ameeleza kuwa mradi huo utajenga jengo ambalo litakuwa na matundu manne ya vyoo, ofisi moja, sehemu ya kukatia tiketi na sehemu ya kupumzika abiria.

Ameeleza kuwa michoro na makadirio halisi ya mradi huo bado havijaletwa kutoka TEMESA Makao Makuu lakini wamepokea mchoro wa awali, mkandarasi wa mradi huo na maelekezo ya kuanza kwa ujenzi huo.

Kwa upande wake, Bwana Christopher Antony, dereva wa pikipiki katika eneo hilo amemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa kutoa maelekezo na kuyafuatilia kuona utekelezaji wake.

“Mheshimiwa usingefika hapa usingejua gharama hii wanayotaka kutumia hapa kwenye huu mradi, jengo hili ni dogo sana ukilinganisha na gharama wanayosema itatumika” alisema Bwana Antony.

Aidha Bwana Antony amewataka watendaji kufanya kazi kwa uadilifu ili kulinda fedha za umma zinazotumika kwenye miradi.

Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa aliambatana na Mkuu wa Wilaya ya Musoma Dokta Alfany Haule na watendaji wa TEMESA na viongozi wengine. 

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa