• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC afungua mgodi wa Kunanga

Posted on: October 11th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mungiya Mzee leo tarehe 10 Oktoba, 2022 ametembelea Mgodi wa Dhahabu wa Kunanga uliopo katika eneo la Kinyambwiga, Wilaya Bunda na kuruhusu uchimbaji wa madini katika mgodi huo uendelee.

Mheshimiwa Mzee ametoa kibali hicho kufuatia baadhi ya wamiliki wa ardhi wa eneo hilo kuingia makubaliano na mikataba na mmiliki wa lesseni za uchimbaji katika eneo hilo na kuruhusu uchimbaji kuendelea bila migogoro iliyokuwepo hapo awali.

“Nimetoa kibali muendelee na shughuli za uchimbaji hapa kwa kufuata sheria na taratibu za uchimbaji wa madini zilizowekwa na Serikali” alisema Mheshimiwa Mzee.

Aidha, amemtaka Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Mara Mhandisi Joseph Kumburu kutoa elimu kwa wachimbaji hao kuhusu sheria na taratibu mbalimbali za uchimbaji wa madini kwa wachimbaji wote wa eneo hilo.

Mkuu wa Mkoa pia amewataka wananchi ambao hawajakubaliana na mwenye lesseni ya uchimbaji katika eneo hilo, kuendelea na shughuli zao za kawaida bila kubughudhiwa na mwenye lesseni.

Mheshimiwa Mzee pia ametoa siku saba kuanzia tarehe 11 Oktoba, 2022 kwa wachimbaji wadogo kusajiri mashimo, klasha na maduala kwa mujibu wa sheria na taratibu za madini.

Mheshimiwa Mzee ameiagiza Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Bunda pamoja na Ofisi ya Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Mara kusimamia usajiri huo kabla ya kuendelea kuchimba madini katika eneo hilo.

Akizungumza katika kikao hicho, Diwani wa Kata ya Guta Mheshimiwa Kigno Nyakimori ameeleza kuwa kwa sasa wachimbaji wa eneo hilo wanaishi maisha magumu kufuatia kufungwa kwa mgodi huo na kumuomba Mkuu wa Mkoa kuruhusu uchimbaji uendelee.

Mheshimiwa Nyakimori ameeleza kuwa wananchi waliokataa kuingia makubaliano na mwenye lesseni ya uchimbaji wamefanya hivyo kwa kuwa wanataka haki itendeke maeneo yao yakitumika na mwenye lesseni ya uchimbaji.

Ameeleza kuwa wananchi hao walianzisa vurugu baada ya kuona hamna muafaka na mwenye lesseni lakini kutokana na makubaliano yaliyofikiwa hategemei kuwa na vurugu tena katika eneo hilo.

Mheshimiwa Mzee amewataka wachimbaji hao kutodanganyika na watu wanaopita na kuwapotosha kuhusiana na mmiliki wa lesseni za madini na uhalali wake wa kuchimba madini katika eneo hilo.

Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa aliambatana na Katibu Tawala wa Mkoa, Kamati ya Usalama ya Mkoa na Wilaya ya Bunda, maafisa kutoka Ofisi ya Afisa Madini Mkazi na Halmashauri ya Mji wa Bunda.

Serikali ya Mkoa wa Mara iliufunga mgodi huo tarehe 13 Aprili, 2022 kufuatia vurugu iliyokuwa imejitokeza na wananchi kumjeruhi askari polisi baada ya polisi kufika eneo hilo kutuliza vurugu zilizokuwepo na baadhi ya wananchi kuwashambulia.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa