• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC aagiza uchunguzi wa miradi Rorya

Posted on: July 22nd, 2022

RC AAGIZA UCHUNGUZI WA MIRADI RORYA  

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi amemwagiza Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara kuunda kamati ya kuchunguza miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Rorya.  

Mkuu wa Mkoa ametoa kauli hiyo baada ya kutembelea baadhi ya miradi na kushiriki katika kikao cha Baraza la Madiwani kwa ajili ya kujibu Hoja za Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali (CAG) leo tarehe 15, 2022.

“Nitataka Katibu Tawala uunde timu ya uchunguzi itusaidie kuchunguza miradi yote ambayo haijatekelezwa vizuri na inayolalamikiwa na wananchi wa Wilaya ya Rorya ili kujiridhisha” alisema Mheshimiwa Hapi.

Miradi itakayochunguzwa ni pamoja na mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Rorya, jengo la ofisi za Halmashauri,  ukumbi wa Halmashauri pamoja na ujenzi wa kivuko cha watembea kwa mguu katika daraja la Mto Mori kilichotekelezwa na Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA).

Katika Hospitali ya Wilaya ya Rorya, ililetewa fedha za kujenga majengo saba ya awali bilioni 1.5 ambazo ziliisha bila majengo kukamilika na serikali iliongeza tena milioni 300 lakini majengo hayo mpaka leo hayajakamilika.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa Hospitali hiyo pia ililetewa shilingi milioni 500 za kujenga wodi tatu lakini fedha zimeisha lakini majengo hayo hayajakamilika.

Mheshimiwa Hapi pia amebaini gharama za mafundi wa kujenga wodi hizo ni asilimia 20 ya vifaa vyote jambo ambalo ni kinyume na mwongozo wa serikali wa asilimia 15 ya gharama za vifaa.

Akiwa katika Hospitali hiyo, pia Mheshimiwa Hapi amekagua mradi wa ujenzi wa nyumba za watumishi wa hospitali hiyo three in one ambao upo katika hatua za ukamilishaji na mradi wa ujenzi wa mochwari, wodi nyingine ambao upo katika hatua za utekelezaji.

Mheshimiwa Hapi ameagiza Halmashauri ya Wilaya ya Rorya kufanya mapitio ya mpango wa matumizi ya ardhi katika Hospitali ya Wilaya ya Rorya na kuomba idhini ya Ofisi ya Rais, Tawala za Miko ana Serikali za Mitaa (TAMISEMI) ili hospitali hiyo isiendelee kujenga miundombinu mingine kwenye eneo lenye maji maji wakati eneo zuri lipo.

Mkuu wa Mkoa pia ametembelea jengo la ofisi za Halmashauri pamoja na ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya ambao ulianza kujengwa mwaka 2007 na SUMA JKT hata hivyo jengo la ofisi linatumika wakati ukumbi ulisimama kutokana na kuishiwa fedha na kuanza kujengwa tena mwaka 2022 baada ya Serikali kuleta fedha milioni 750 kwa ajili ya kukamilisha mradi huo.

Mheshimiwa Hapi ameikemea Halmashauri hiyo baada ya kutaarifiwa kuwa Halmashauri hiyo imeomba fedha za nyongeza milioni 250 kukamilisha jengo hilo; “kwa hatua hii mlipofikia na fedha mnayosema imebakia, mnahitaji shilingi milioni 250 kwa ajili ya nini?” alisema Mheshimiwa Hapi.

“Hili jengo (ofisi za Halmashauri) mpaka leo halijakamilika, kuna jenerata na strongroom kwa ajili ya kuhifadhia mitihani ilitakiwa kuwekwa havijawekwa, vigae vimebanduka na halijakabidhiwa muda wote huo” alisema Mhehsimiwa Hapi.

Kuhusu kivuko, Mheshimiwa Hapi amepokea malalamiko kutoka kwa wananchi wanaolalamikia kivuko hicho kutumia gharama kubwa ukilinganisha.

“Ninataka hiki kivuko nacho tukichunguze kujua uhalali wa kutumia zaidi ya milioni 70 katika kivuko hicho ambacho wananchi wanakilalamikia” alisema Mheshimiwa Hapi.

Akitoa taarifa ya miradi hiyo kwa Mkuu wa Mkoa, Mhandisi wa Halmashauri hiyo Mhandisi Erick Mwita ameeleza kuwa awali hospitali hiyo ililetewa kiasi cha bilioni 1.5 kwa ajili ya kujenga majengo saba ambayo hayakukamilika na baadaye ikaletewa shilingi milioni 300 kukamilisha lakini bado majengo hayo hayajakamilika.

Mhandisi Mwita ameeleza kuwa baadaye Hospitali hiyo ilipokea fedha shilingi milioni 500 kwa ajili ya kujenga wodi tatu ambazo pia hazijakamilika, vifaa vimenunuliwa lakini hamna fedha za kulipa mafundi ili kuendelea na kazi.  

“Katika ujenzi wa wodi hizi, Halmashauri ilipata gharama kubwa ya kuleta vifaa eneo la ujenzi wakati wa masika kutokana na ubovu wa barabara na msingi kutumia fedha nyingi kutokana na eneo kuwa na maji maji” alisema Mhandisi Mwita.

Aidha, Mhandisi Mwita ameeleza kuwa serikali imeleta tena fedha nyingine kwa ajili ya kujenga majengo mengine ambapo ujenzi wake unaendelea.

 Akiwa katika Kikao cha Baraza la Madiwani, Mheshimiwa Hapi ameitaka Halmashauri hiyo kukusanya madeni na kuongeza jitihada katika ukusanyaji wa mapato ya ndani ya Halmashauri hiyo. Halmashauri hiyo ilikuwa na hoja 68 na hoja 10 zilijibiwa na kufungwa, hoja nyingine zipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Mtambi afungua kambi ya madaktari bingwa na bobezi 64 Mara

    June 23, 2025
  • Watumishi wa Sekretarieti ya Mkoa wa Mara wapatiwa mafunzo

    June 20, 2025
  • Mara mshindi wa pili UMITASHUMTA 2025

    June 18, 2025
  • Zingatieni miongozo ya kilimo cha tumbaku- Dkt. Haule

    June 18, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa