• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC aagiza uchunguzi wa madeni Serengeti

Posted on: July 22nd, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi amemuagiza Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara  kuunda timu ya kuchunguza uhalisia na uhalali wa madeni katika Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti.

Mheshimiwa Hapi ametoa agizo hilo leo tarehe 16 Julai, 2022 katika kikao maalum cha Baraza la Madiwani la kujadili hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka 2020/2021.

“Nataka timu ije kuchunguza uhalisia na uhalali wa deni lenye thamani ya bilioni 4.1 linalosemekana lipo katika Halmashauri ili kubaini limetokana na nini, uhalali wake ili kama Mkoa tujiridhishe na deni hili” alisema Mheshimiwa Hapi.

Aidha, amemuagiza Katibu Tawala wa Mkoa kuhakikisha timu inayokagua miradi iliyokwama katika Halmashauri ipite na Kituo cha Afya Machochwe kilicholetewa fedha milioni 500 ambazo zimeisha na kituo hakijakamilika.

“Ninataka uchunguzi katika huo mradi, nchi nzima milioni 500 zinakamilisha ujenzi wa Kituo cha Afya, lakini Serengeti wanasema zimeisha na zinahitajika nyingine milioni 150 kukamilisha mradi huo, hii haikubaliki” alisema Mheshimiwa Hapi.

Wakati huo huo, Mkuu wa Mkoa ameipongeza Shule ya Sekondari ya Natta kwa kushika nafasi ya 11 kitaifa kwenye matokeo ya Kidato cha Sita ya mwaka 2022 yaliyotangazwa hivi karibuni.

“Mimi nitatoa shilingi 500,000 kwa ajili ya kuwapongeza walimu, lakini ninataka Mkuu wa Wilaya ongea na wadau mbalimbali kwa ajili ya kuwapongeza walimu wa Shule ya Sekondari Natta kwa kufanya vizuri” alisema Mheshimiwa Hapi. 

Awali, Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Mheshimiwa Ayoub Mwita Makuruma ameeleza kuwa Halmashauri hiyo ina madeni makubwa yaliyosababisha na uzembe wa viongozi waliokuwepo katika Halmashauri hiyo.

“Cha kushangaza kuhusu haya madeni kwa sehemu kubwa yametengenezwa katika kipindi ambacho Halmashauri hiyo ikiwa katika hali nzuri kifedha, jambo ambalo linazua maswali kwa nini hayakulipwa” ameeleza Mheshimiwa Makuruma.

Ameelezea wasiwasi wa madeni hayo kuwa huenda yalitengenezwa tui li kuchukua fedha za Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti.

Mheshimiwa Makuruma amemuomba Mkuu wa Mkoa kuisaidia Halmashauri hiyo kwa kuwaondoa wakuu wa Idara na Vitengo waliokaa katika nafasi zao kwa muda mrefu.

Suala la madeni liliongelewa pia na madiwani waliopata nafasi ya kuchangia katika kikao hicho na kuonyesha kutoridhika kwao na deni hilo la Halmashauri.   

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti Bwana Kivuma Msangi ameeleza kuwa Halmashauri hiyo kwa mwaka wa fedha 2020/2021 ilikuwa ina hoja 93 na hadi wakati wa kikao hicho 31 zilikuwa zimejibiwa na zimefungwa, hoja 29 zinazoendelea kujibiwa na hoja nyingine 33 hazijaanza kutekelezwa.

Bwana Msangi ameeleza kuwa Halmashauri pia ilikuwa na maagizo mawili ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Serikali za Mitaa (LAAC) ambapo moja limejibiwa kikamilifu na moja linaendelea kujibiwa kipengele kinachohusu mwekezaji Grumeti kulipa ada ya uwindani milioni 500 badala ya milioni 200 wanazolipa sasa.

Bwana Msangi ameeleza kuwa katika ukaguzi huo Halmashauri hiyo ilipata hati safi ya ukaguzi na hiyo ni mwendelezo ambapo kwa miaka mitatu mfulilizo imekuwa ikipata hati safi za ukaguzi.

Kikao hicho kilihudhuriwa na Mkuu wa Wilaya ya Serengeti, Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa, Katibu Tawala wa Wilaya ya Serengeti, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Serikali za Mitaa, wajumbe wa Kamati ya Ulinzi ya Mkoa na Wilaya, wajumbe wa Baraza la Madiwani, Wakaguzi kutoka ofisi ya CAG, watumishi wa Halmashauri.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa