• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RAS akagua miradi ya Elimu Butiama

Posted on: February 19th, 2025

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Gerald Musabila Kusaya leo amefanya ziara katika Halmashauri ya Wilaya ya Butiama na kukagua ujenzi unaoendelea katika Shule ya Sekondari ya Butuguri na Shule ya Amali ya Mkoa wa Mara.

Katika Shule ya Sekondari ya Butuguri, Bwana Kusaya amekagua ujenzi wa miundombinu ya madarasa, mabweni na matundu ya vyoo kwa ajili ya mapaokezi ya wanafunzi wa kidato cha tano Julai, 2025 na kupongeza kwa kazi nzuri iliyofanyika na kumtaka Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Butiama kuongeza kasi ya ujenzi.

Aidha, Katibu Tawala wa Mkoa amemuagiza Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Mgango- Kiabakari kuhakikisha shule hiyo inapata maji ya uhakika kabla ya kupokea wanafunzi wa kidato cha tano.

Katika Shule ya Amali ya Mkoa wa Mara, Katibu Tawala wa Mkoa amekagua mradi huo unaendelea kujengwa katika Kijiji cha Butiama na kupongeza kwa kazi inayoendelea na kumtaka Mkurugenzi wa Wilaya ya Butiama kuongeza kasi ya ujenzi ili shule hiyo ianze kuchukua wanafunzi wa kidato cha kwanza Januari, 2026.

Aidha, Bwana Kusaya amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Butiama kufanya utaratibu wa kuongeza eneo zaidi kwa ajili ya upanuzi wa shule hiyo ili kuweza kukidhi mahitaji halisi ya Shule za Amali za Mkoa.

“Hili eneo la ekari 40 ninaliona ni dogo, shule za amali zinakuwa na majengo mengi zaidi ikiwemo nyumba za walimu, hili eneo halitatosha, fanyeni utaratibu mliongeze” amesema Bwana Kusaya.

Bwana Kusaya amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Butiama kukamilisha miradi hiyo ndani ya miezi miwili na atarudi tena kukagua miradi hiyo tarehe 17 Aprili, 2025 ili kuona maendeleo yake.

Kwa upande wake, Mkuu wa Shule ya Sekondari Butuguri Mwal. Nyamtelele Christopher amesema kwa mwaka wa fedha 2024/2025 shule hiyo imepokea jumla ya shilingi 510,448,303.78 kwa ajili ya ujenzi wa mabweni matatu, vyumba vya madarasa saba, matundu nane ya vyoo na fedha za ukamilishaji wa darasa moja.

Mwal. Christopher amesema fedha hizo zimetoka katika vyanzo mbalimbali ikiwemo EP4R II, Serikali Kuu na SEQUIP na zilipokelewa kwa awamu tofauti tofauti na mpaka sasa bweni moja na vyumba vinne vya madarasa vimekamilika, huku mabweni mawili yapo kwenye hatua za msingi.

Mwal. Christopher amesema ujenzi wa matundu ya vyoo, vyumba vya madarasa vinne vipo katika hatua mbalimbali za ukamilishaji na wanategemea kukamilisha mradi huo ndani ya miezi miwili kuanzia sasa.  

Mwal. Christopher amesema shule hiyo kwa sasa inachangamoto ya upatikanaji wa maji kwa ajili ya ujenzi na matumizi ya wanafunzi wa kutwa wanaosoma hapo na kuwa wanatumia gharama kubwa kununua maji kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu hiyo.

Kwa upande wake, Mkuu wa Shule ya Sekondari Butiama Mwal. Grace Isomba ambaye pia ni msimamizi wa mradi wa ujenzi wa Shule ya Amali Mkoa wa Mara amesema mradi huo ulipokea fedha shilingi bilioni 1.6 mwishoni mwa mwaka wa fedha 2023/2024.

Mwal. Isomba amesema fedha hizo ni kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu 13 ikiwemo vyumba vya madarasa (08), jengo la utawala, maabara mbili, ofisi za walimu mbili, nyumba moja ya walimu, maktaba, chumba cha Tehama, Mabweni manne, bwalo na jiko, vyoo matundu 08, karakana za ufundi tatu na tenki la maji.

Mwa. Isomba amesema mpaka sasa mradi huo umetumia shilingi 353,491,943,04 na kubakiwa na shilingi 1,246,508,056.96 kwa ajili ya ukamilishaji wa mradi huo.

Katika ziara hiyo, Katibu Tawala wa Mkoa aliambatana Maafisa kutoka Sekretarieti ya Mkoa wa Mara, Katibu Tawala wa Wilaya ya Butiama, Mkurugenzi wa Halmashauri na baadhi ya watumishi wa Halmashauri hiyo.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa