• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Naibu Waziri Mkuu kuongoza Mazishi ya Mtendaji Mkuu TANESCO

Posted on: April 15th, 2025

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Mashaka Biteko anategemewa kuwaongoza waombolezaji katika mazishi ya aliyekuwa Mkurugenzi Mwendeshaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Mhandisi Gissima Nyamo-Hanga yatakayofanyika tarehe 16 Aprili, 2025 katika eneo la Mikungani, Wilaya ya Bunda.

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuhani msiba wa Mhandisi Nyamohanga, Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi amesema marehemu NyamoHanga alikuwa mzalendo na mpenda maendeleo ya nchi na kifo chake ni msiba mkubwa kwa wananchi wa Mkoa wa Mara na Watanzania.  

“Mhandisi Nyamohanga alikuwa mdau mkubwa wa maendeleo wa Mkoa wa Mara na ametusaidia sana katika kupitia Wakala wa Umeme Vijijini (REA) kusambaza umeme katika vitongoji vya Mkoa wa Mara na maeneo ya wachimbaji wadogo wadogo ambayo awali yalikuwa hayapati umeme.

Mhe. Mtambi amesema Mhandisi amesaidia pia kupeleka umeme katika Shule ya Amali ya Mkoa inayoendelea kujengwa katika Wilaya ya Butiama na amesaidia pia kurejesha umeme kwa haraka wakati wa maafa yaliyosababishwa na mvua ya upepo yaliyotokea Manispaa ya Musoma kwa kuhakikisha TANESCO inarejesha umeme eneo lililoathirika haraka.  

Mhe. Mtambi ametoa pole kwa viongozi na watendaji wa Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Wizara ya Nishati, TANESCO na wafiwa wote wanaohusika katika msiba huo na kuwataka waombolezaji kuendelea kumuenzi Mhandisi Nyamohanga kwa kutenda mambo mazuri kwa Taifa letu.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Kanda ya Ziwa wa TANESCO Mhandisi Satco Nombo amesema kwa sasa maandalizi muhimu kwa ajili ya mazishi ya Mhandisi Nyamohanga katika eneo la Migungani, Wilaya ya Bunda yanaendelea vizuri.

Mhandisi Nyamohanga amesema viongozi, menejimenti na watumishi kutoka TANESCO na Wizara ya Nishati, taasisi nyingine za Serikali na wanafamilia wanaotarajiwa kushiriki mazishi hayo wanatarajiwa kufika Bunda kuanzia tarehe 15 Aprili, 2025.

Mhandisi Nombo amesema aliyekuwa Dereva wake ambaye pia alifariki katika ajali hiyo Ndugu Mujahir Mohamed Haule tayari amesafirishwa kwenda Mkoa wa Pwani na amezikwa tarehe 14 Aprili, 2025.

Mhandisi Nyamohanga na dereva wake walifariki katika ajali iliyotokea usiku wa kuamkia tarehe 13 Aprili, 2025 katika Kata ya Nyatwali, jirani na geti kuu la Hifadhi ya Taifa ya Serengeti lililopo eneo la Ndabaka, Wilaya ya Bunda.

 Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa aliambatana na Kamati ya Usalama ya Mkoa, Kamati ya Usala ya Wilaya ya Bunda, baadhi ya watumishi wa Sekretarieti ya Mkoa wa Mara na Halmashauri ya Mji wa Bunda.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa