• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mzee awataka walimu kuwa wabunifu

Posted on: January 6th, 2023

MZEE AWATAKA WALIMU KUWA WABUNIFU

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mungiya Mzee leo amewataka walimu wa shule mbalimbali katika Mkoa wa Mara kuwa wabunifu na kujiongeza katika utekelezaji wa majukumu yao.

Mheshimiwa Mzee ametoa wito huo wakati akifanya ziara ya kupokea vyumba vya madarasa katika Wilaya ya Serengeti na kuwaelekeza walimu kuanzisha miradi mbalimbali ya kuongeza mapato ya shule ili kuweza kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili.

“Walimu wetu hawana ubunifu, wa kujiongezea au kufanya mabadiliko katika shule zetu, Shule zinaweza kufanya biashara ndogo ndogo na kupata pesa za kuweza kutatua changamoto ndogo ndogo zinazowakabili” alisema Mheshimiwa Mzee.

Mheshimiwa Mzee ameeleza kuwa miradi itakayoanzishwa inaweza kutoa huduma na elimu kwa vitendo kwa walimu na wanafunzi wanaosoma katika shule hizo na wananchi wanaowazunguka maeneo ya shule.  

Aidha, amewataka walimu kutumia fursa ya kuwa na wanafunzi wengi kubuni miradi ambayo itawasaidia kupata fedha za kutatua changamoto mbalimbali pindi zinapojitokeza.

Wakati huo huo, Mkuu wa Mkoa amewataka walimu na wasimamizi wa elimu kusimamia suala la uboreshaji wa mazingira ya shule kwa kupanda miti, maua, matunda na kuyasawazisha maeneo ya shule na kuzuia mmomonyoko wa udongo katika shule zao ili wanafunzi waweze kupita vizuri.

“Mazingira yanatakiwa yawe mazuri ili wanafunzi wapende kwenda shule na wakienda wajifunze kitu kutokana na ubunifu katika kuongeza mapato na kutunza mazingira” alisema Mheshimiwa Mzee.   

Katika ziara hiyo, kati ya shule tano alizotembelea, Shule ya Sekondari Rigicha pekee ilitoa taarifa ya kuwa na mradi wa shule wa ufugaji wa nyuki, lakini shule nyingine zilitoa taarifa ya kuwa na mpango wa kuanzisha miradi lakini bado hawajapata mtaji wa biashara.

Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa aliambatana na Mkuu wa Wilaya ya Serengeti, Katibu Tawala sehemu ya Elimu, Katibu Tawala sehemu ya Miundombinu, Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Serengeti, watumishi ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, Menejimenti ya Wilaya ya Serengeti na viongozi wa CCM Wilaya ya Serengeti.  

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa