• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtanda azindua mradi wa Maji wa Bilioni 2.7

Posted on: November 10th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Said Mohamed Mtanda leo amezindua mradi wa maji wa Bulinga/Busungu uliopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Musoma unaosimamiwa na Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) kwa gharama ya shilingi bilioni 2.7.

“Huu ni mradi mkubwa sana ambao unawawezesha wananchi kupata maji safi na salama yenye uhakika, rai yangu tuutunze ili udumu ili wananchi wapate manufaa yaliyotegemewa na mradi huu” amesema Mhe. Mtanda.

Mhe. Mtanda ameitaka RUWASA kushughulikia kero ya mita za maji zinazolalamikiwa na wananchi na kuwapitia wale wanaolalamika na kuangalia matumizi yao sahihi ya maji ili walipe hiyo wakati RUWASA inajipanga kuwabadilishia mita hizo zinazolalamikiwa.

Aidha, Mheshimiwa Mtanda ameiagiza RUWASA kuanzisha utaratibu maalum wa kusikiliza kero za wananchi kuhusu maji ikiwa ni pamoja kuwatembelea katika vijiji vyao na kusikiliza kero zao kuhudu huduma za maji.

Mhe. Mtanda pia ameiagiza RUWASA kuongeza vituo vya kuchotea maji katika Kijiji cha Busungu na kuitaka RUWASA kuangalia namna ya kuweza kuwahamasisha wananchi wengi zaidi kuingiza maji majumbani hata kama kwa mkopo utakaorejeshwa taratibu.

Mkuu wa Mkoa pia amewataka wananchi wenye uwezo kuunganisha maji majumbani ili kupata huduma hiyo kwa ukaribu zaidi na kutumia muda wao kufanya shughuli za maendeleo.

Kwa upande wake, Meneja wa RUWASA Wilaya ya Musoma Mhandisi Edward Sironga ameeleza kuwa mradi huo ulianza kutekelezwa Julai, 2018 na umekamilika Julai, 2021 kwa ufadhili wa Mfuko wa Maji wa Taifa (NWF)  na utawanufaisha wakazi 16, 443 kutoka vijiji vitano vya eneo hilo.

Mhandisi Sironga amevitaja vijiji vitakavyonufaika kuwa ni pamoja na Bulinga, Bujaga, Busungu, Bukima na Kikwerege vilivyopo katika Kata za Bulinga, Bukima na Rusoli na kutokana na uwingi wa maji mradi huu unapanuliwa nkuelekea Kata ya Bwasi ambapo wakazi wapatao 12,072 watahudumiwa.

“Mahitaji ya maji kwa wakazi wanaohudumiwa na mradi ni lita 411,075 kwa siku wakati chanzo cha maji cha mradi huo kinauwezo wa kutoa lita 1,344,000 kwa siku ambayo ni sawa na mara tatu na nusu ya mahitaji ya wananchi” amesema Mhandisi Sironga.

Bwana Sironga ameeleza kuwa mradi huo umejenga matenki mawili ya maji, mtandao wa mabomba ya maji yenye urefu wa kilomita 28.11 na majengo mawili kwa ajili ya ofisi ya jumuiya ya watumia maji (BULISUMAKWI).

Aidha, Bwana Sironga ameeleza kuwa pamoja na ukubwa wa mradi na wingi wa maji, mradi huo umefanikiwa kuwaunganisha wateja wa majumbani 185 na wengine wanachota maji katika vituo vya kuchotea maji.

Wakati huo huo, Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Said Mohamed Mtanda ameitembelea na kukagua ujenzi wa Sekondari mpya katika Kijiji cha Wanyere na kuipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Musoma kwa utekelezaji wa mradi huo.

Aidha, Mkuu wa Mkoa ameielekeza Halmashauri hiyo kuwataka mafundi waongoze kasi ya ujenzi ili shule hiyo iweze kuanza kuchukua wanafunzi kuanzia Januari, 2024.

Katika ziara hiyo Mkuu wa Mkoa aliambatana na Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Musoma Mhe. Juma Chikoka (Mkuu wa Wilaya ya Rorya), Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Musoma, Kamati ya Siasa ya Wilaya ya Musoma Vijijini, watendaji na baadhi ya madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma. 

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa