• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtanda awataka Mikomariro na Remng'orori kudumisha amani

Posted on: October 25th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Said Mohamed Mtanda leo amefanya ziara katika eneo lenye mgogoro mpakani mwa Wilaya za Serengeti na Bunda na kuwataka wananchi wa vijiji vya Mikomariro kilichopo Wilaya ya Bunda na Remng’orori kudumisha amani na usalama wakati Serikali inatafuta suluhu ya kudumu ya mgogoro huo.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika eneo linalogombaniwa na wananchi wa vijiji hivyo, Mhe. Mtanda ameelezea kusikitishwa kwake na vitendo vya wananchi kuendelea kuhatarisha amani ya eneo hilo wakati Serikali tayari imechukua hatua mbalimbali ili kuendelea kushughulikia mgogoro huo.

“Ninyi wananchi wa Remng’orori na Mikomariro ndio mnauwezo wa kuamua kuumaliza mgogoro huu, hapa hatutafuti mshindi, mshindi hapa ni amani na usalama katika eneo hili, hicho kikiwa ndio kipaumbele chetu, mgogoro huu utaisha”  amesema Mhe. Mtanda.

Mhe. Mtanda pia amezungumza na viongozi wa serikali za vijiji na wazee wa vijiji hivyo na kuwataka kuleta mapendekezo Serikalini ya namna bora ya kumaliza mgogoro huo na kuwaomba viongozi hao kukutana kwenye kikao cha pamoja ili kutoa makubaliano yenye lengo la kumaliza mgogoro huo.  

“Kwa sasa ninaomba vigingi vilivyowekwa na Serikali viheshimiwe na wananchi wote na kila mwenye haki yake katika mgogoro huu ataipata haki yake, sio kwa kupigana na kuuana bali kwa kufuata sheria na taratibu” amesema Mhe. Mtanda.

Mhe. Mtanda amewaonya viongozi , watendaji  na wananchi wote wanaoendelea kuuchochea mgogoro huo kuwa Serikali ipo makini na itawachukulia hatua za kisehria wahusika wote wa mgogoro huo.

Aidha, Mhe. Mtanda ameeleza kuwa zoezi la upangaji wa matumizi bora ya ardhi katika vijiji hivyo limesitishwa hadi hapo suluhu ya kudumu ya mgogoro huo uliodumu kwa muda mrefu itakapopatikana.

Kwa upande wao, viongozi na wazee wa vijiji hivyo wamekubali kukutana kwenye kikao cha pamoja cha kutafuta suluhu ya mgogoro huo katika kikao kitakachohudhuriwa pia na viongozi na watendaji wa Serikali.

Wananchi wa eneo hilo wanagombea eneo lililopo mpakani kati ya Wilaya ya Butiama, Bunda na Serengeti uliodumu kwa muda mrefu hata hivyo kwa siku za hivi karibuni mgogoro upo zaidi kati ya wananchi wa Wilaya za Bunda na Serengeti.  

 Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa aliambatana na Kamati ya Usalama ya Mkoa, baadhi ya viongozi wa Chama cha Mapinduzi, Wakuu wa Wilaya na Kamati za Usalama za Wilaya za Bunda na Serengeti, watumishi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na Ofisi ya Ardhi Mkoa, viongozi na watendaji wa Halmashauri za Wilaya za Bunda na Serengeti.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa