• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtanda ataka uchunguzi Kituo cha Afya Machochwe

Posted on: November 9th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Said Mohamed Mtanda leo tarehe 31 Oktoba, 2023 amefanya ziara katika Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti na kuagiza wakaguzi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara kuchunguza matumizi ya fedha katika ujenzi wa Kituo cha Afya Machochwe.

Mhe. Mtanda ametoa agizo hilo baada ya kukagua na kupokea malalamiko ya viongozi na wananchi kuhusiana na kutoridhishwa na utekelezaji wa mradi huo ulioanza kutekelezwa tangu mwaka 2021 kwa gharama ya shilingi milioni 520 na mpaka sasa hamna jengo hata moja lililokamilika.

“Kama kuna aliyehusika kukifanya kituo hiki kisifikie malengo, kwanza tushughulike nae (kumfikisha kwenye vyombo vya sheria) kabla hatujatafuta fedha nyingine….Mkoa wa Mara hautageuzwa tena kuwa shamba la Bibi!” amesema Mhe. Mtanda.

Wakati huo huo, Mhe. Mtanda ametoa mwezi mmoja kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti kuweza kukamilisha majengo ya wagonjwa wa nje (OPD) na maabara ili yaanze kutumika kutoa huduma kwa wananchi. 

Aidha, Mhe. Mtanda amewapongeza wananchi wa Kata ya Machochwe kwa kutoa mchango wa viashiria na fedha taslimu wakati wa ujenzi wa mradi huo vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 20.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Serengeti Mhe. Dkt. Vincent Mashinji ameeleza kuwa Kamati ya Usalama ya Wilaya ilitembelea mradi huo na kuagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (PCCB) kufanya uchunguzi wa mradi huo.

“Hilo jalada la uchunguzi mpaka sasa PCCB wanalifanyiakazi….. lakini limechukua muda mrefu sana suala hili kuweza kuhitimishwa” amesema Mhe. Mashinji.

Mhe. Mashinji ameeleza kuwa wakati wa utekelezaji wa mradi huo Kamati ya Manunuzi inayowahusisha wananchi haikuhusishwa katika manunuzi ya vifaa vya mradi huo.

Dkt. Mashinji amesema vifaa vyote vilinunuliwa na Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti bila kufuata mwongozo wa force account na vifaa vya ujenzi vilivyonunuliwa ni vingi kuliko mahitaji ya mradi huo.

Aidha, Mhe. Mashinji ameeleza kuwa baadhi ya vifaa vya mradi huo vitatumika kukamilisha majengo yanayoendelea kujengwa na kuhamishiwa katika miradi mingine kwa utaratibu wa kurudishia fedha.

Awali akitoa taarifa za mradi huo, Mganga Mfawidhi wa zahanati ya Machochwe ameeleza kuwa kwa sasa fedha iliyobakia ni zaidi ya shilingi milioni 14 na vifaa vya zaidi shilingi milioni 30. 

Aidha, taarifa hiyo ilionyesha kuwa Kituo hicho kinahitaji shilingi milioni 151 ili kuweza kukamilika na kuanza kutoa huduma kwa wananchi.

Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Mkoa wa Mara alitembelea pia mradi wa maji wa Kenyamonte, Shule ya Msingi Ikorongo, Shule ya Sekondari ya Morotonga na kuzungumza na wananchi katika Kijiji cha Park Nyigoti. 

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa