• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi: wanafunzi wote wapate chakula shuleni ifikapo Januari, 2025

Posted on: September 19th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo ameongoza kikao cha viongozi na watendaji wa Mkoa wa Mara kuhusu utoaji wa chakula shuleni na kuwataka viongozi, wazazi na wadau wote kuhakikisha kuwa wanafunzi wote wa Mkoa wa Mara wanapata chakula cha mchana shuleni kuanzia Januari, 2025.

Mhe. Mtambi ametoa agizo hilo leo wakati akizungumza katika kikao hicho na kuwataka viongozi wa Serikali wa Mkoa wa Mara kusimamia maelekezo hayo na kuhakikisha wanafunzi wote wanapata angalau mlo wa mmoja wa mchana wakiwa shuleni ili waweze kujifunza vizuri.

“Haikubaliki kuendelea kuwafanyia ukatili wanafunzi kwa kuwashindisha na njaa kwa sababu tu viongozi na wazazi tumeshindwa kutimiza wajibu wetu katika kutoa chakula shuleni” amesema Mhe. Mtambi na kuwataka wazazi na walezi wote kuchangia ili wanafunzi wapate chakula shuleni.

Mhe. Mtambi amesema chakula kinachochangiwa sio cha ziada bali ni chakula ambacho mtoto akiwa nyumbani angekula na hivyo ni wajibu wa wazazi na walezi wa wanafunzi kutoa chakula hicho ili wanafunzi wapate chakula wakiwa shuleni.

Kanali Mtambi amezitaka Halmashauri kuhakikisha kuwa shule zote zenye maeneo au mashamba zitumie maeneo hayo kulipa na kupata chakula ili kuwasaidia wazazi katika mchango wa chakula na kuwafundisha wanafunzi kwa vitendo kuhusu kilimo na shughuli za kujitegemea.

Mhe. Mtambi amewataka wadau wa elimu kuchangia kwa hali na mali ili kuhakikisha wanafunzi wote wanapata chakula shuleni na Halmashauri kutunga sheria ndogo za kusimamia utoaji wa chakula shuleni ili wazazi/walezi wanaokaidi kuchangia wachukuliwe hatua za kisheria.

Mhe. Mtambi amezitaka Halmashauri kuhakikisha kuwa chakula kinachochangwa na wazazi kinahifadhiwa vizuri na kwa usalama katika maeneo ya shule na kushughulikia wasiwasi wa wananchi kuwa chakula kinachochangwa kinatumika vibaya na walimu.

Kwa upande wake, Kaimu Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Elimu Bi. Judith Mrimi amesema programu ya chakula shuleni ni muhimu kwa ajili ya kuongeza udahili na usajili wa wanafunzi, mahudhurio, usikivu na kuinua ufaulu wa wanafunzi katika mitihani.

Bibi Mrimi amesema kwa mujibu wa mwongozo wa Kitaifa wa Utoaji wa Huduma ya Chakula na Lishe kwa wanafunzi wa Elimumsingi, wanafunzi wote wa shule za kutwa za msingi na sekondari wanapaswa kupata huduma ya chakula cha mchana shuleni.

Bibi Mrimi amesema mwongozo huo umebainisha kuwa chakula kwa ajili ya wanafunzi kitapatikana kutoka kwa Serikali kwa wanafunzi wanaosoma shule za bweni na kwa shule za kutwa michango ya chakula itatoka kwa wadau wa elimu, sekta binafsi, wabia wa maendeleo, mashamba na bustani za shule, michango ya wazazi.

Bi Mrimi amesema kuwa mwongozo huo umeainisha michango ya chakula shuleni inaweza kuwa ni pamoja na michango ya vyakula, fedha taslimu, nguvu kazi, miundombinu na michango ya uwezeshaji au kuwajengea wananchi uwezo wa kitaalamu.

Bibi Mrimi amesema Halmashauri ni moja ya wadau muhimu wa utoaji wa chakula shuleni na inatakiwa kuweka kwenye mipango yake shughuli za kuhamasisha wazazi na jamii kupitia viongozi wa mitaa au vijiji kushiriki utoaji wa chakula shuleni, udhibiti wa ubora na usalama wa chakula kwa kutoa elimu na kuandaa sheria ndogondogo za utoaji wa chakula shuleni.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa