• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi azipongeza Halmashauri ukusanyaji wa mapato

Posted on: December 12th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo ameongoza kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Mara (RCC) na kuzipongeza Halmashauri ukusanyaji mzuri wa mapato ya ndani ambapo hadi kufikia tarehe 30 Novemba, 2024 Halmashauri hizo zimekusanya shilingi bilioni 16.516 sawa na asilimia 107 ya lengo la makusanyo kwa muda huo.

Akizungumza katika kikao hicho kilichofanyika katika Ukumbi wa Uwekezaji, Mhe. Mtambi amesema makusanyo hayo ni sawa na asilimia 45 ya makusanyo yaliyopangwa kukusanywa katika mwaka wa fedha 2024/2025.

“Ninazipongeza zaidi Halmashauri ya Wilaya ya Tarime na Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti ambazo zimekusanya kwa zaidi ya asilimia 50 ya makusanyo yaliyopangwa kwa mwaka wa fedha 2024/2025” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi ameitaka Halmashauri ya Mji wa Tarime kuweka mikakati vizuri ili kuongeza kasi ya ukusanyaji wa mapato na kuhakikisha inafikia asilimia 100 ya makusanyo hadi kufikia mwisho wa mwaka wa fedha 2024/2025.

Mhe. Mtambi ametumia fursa hiyo kuvipongeza vyama vya siasa vilivyoshiriki uchaguzi katika Mkoa wa Mara kwa ushirikiano walioutoa katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa katika Mkoa wa Mara.

Aidha, amewataka viongozi kuwahamasisha wananchi kutumia vizuri mvua zinazoendelea kunyesha kulima mazao ya chakula na biashara ili kuimarisha uchumi wa familia zao, Mkoa na uchumi wa nchi kwa ujumla.  

Kwa upande wake, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Menejimenti ya Ufuatiliaji na Ukaguzi (MMI) Bwana Marco Maduhu amesema kwa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime ambayo katika mpango wa makusanyo hadi mwisho wa Novemba ilitakiwa kukusanya 4,754,526,589 lakini imefanikiwa kukusanya milioni 6,662,423,141.

“Mwenendo wa makusanyo wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime ni mzuri na hali hii ikiendelea kuna uwezekano wa Halmashauri kukusanya asilimia 100 au zaidi ya bajeti yake yam waka 2024/2025” amesema Bwana Maduhu.

Bwana Maduhu amesema Halmashauri ya Mji wa Tarime imefanikiwa kukusanya asilimia 26 tu ya mpango wake wa makusanyo ya mwaka na kuonya kwamba hali ikiendelea hivi kuna uwezekano Halmashauri kushindwa kufikia lengo la kukusanya mapato kwa asilimia 100 ya bajeti ya mwaka 2024/2025.

Bwana Maduhu amezitaka Halmashauri kuongeza juhudi za kukusanya mapato ya ndani na kuhakikisha wanadhibiti mianya ya upotevu wa mapato, matumizi sahihi ya mfumo wa kukusanyia mapato wa kielekroniki (TAUSI) na kuhakikisha kamati za mapato zinafanyakazi kwa ufanisi na kuzingatia mwongozo wa usimamizi wa mapato ya Halmashauri wa mwaka 2019.

Aidha, Bwana Maduhu amezitaka Halmashauri kuendelea kufanya tathmini ya uwezo wa vyanzo vya mapato vilivyopo na kubuni vyanzo vipya ya mapato na kuzitaka Halmashauri zenye sababu ya msingi zitakazosababisha kushindwa kukusanya kwa mujibu wa malengo kuomba kupunguzia bajeti kabla ya Februari, 2025.

Kikao hicho kimehudhuriwa na Wakuu wa Wilaya, Kamati ya Usalama ya Mkoa, wabunge, viongozi wa dini, viongozi wa vyama vya siasa, Menejimenti ya Sekretarieti ya Mkoa wa Mara, Makatibu Tawala wa Wilaya na viongozi wa taasisi za umma.

Wengine walioshiriki kikao hicho ni Meya na Wenyeviti wa Halmashauri, Wakurugenzi wa Halmashauri, Maafisa Mipango wa Halmashauri, baadhi ya watumishi wa Sekretarieti ya Mkoa wa Mara.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa