• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi awataka wanawake kugombea nafasi za uongozi

Posted on: June 12th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo tarehe 12 Juni, 2025 amezindua kongamano la wamawake wa Kanisa la Tanzania Missionary Revival Church (TMRC) katika eneo la Kigera, Manispaa ya Musoma na kuwataka wanawake kushiriki uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 na kuwania nafasi za uongozi.

Mhe. Mtambi amesema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ameonyesha mfano kuwa viongozi wanawake wanatekeleza vizuri majukumu yake na kuwataka wanawake zaidi kugombea nafasi za ubunge, udiwani katika nafasi hiyo.

“Kwa sasa Mama amewasafishia njia hata ambao walikuwa hawaamini kwa mfano huu Mhe. Rais alioutoa hapa nchini kwa sasa kila mtu anaamini wanawake wanaweza na wanafanya vizuri kuliko wanaume” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amesema wanawake waliopewa nafasi mbalimbali za uwaziri, ubunge na udiwani wanafanya vizuri na kuongeza kuwa hapo baadae inaweza kuwa vigumu kwa wanaume kugombea kwa kuwa wanawake waliopewa nafasi mbalimbali wanafanya vizuri sana.

Mhe. Mtambi amewataka kuliombea Taifa na hususan wakati huo nchi inapoelekea katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 na kuwahamasisha watu wote kushiriki uchaguzi kwa kupiga kura na kuwachagua viongozi na kama wanasifa kugombea katika uchaguzi huo.

Kanali Mtambi amewataka wanawake hao kuihamasisha jamii kudumisha umoja, amani na mshikamano uliopo bila kubaguana kwa misingi ya dini, siasa na makundi yasiyofaa katika jamii na kuihamasisha jamii kuilinda amani na utulivu uliopo hapa nchini.

Mkuu wa Mkoa amewahakikishia wanawake hao kuwa Serikali inatambua na kuuthamini mchango wa madhehebu ya dini na viongozi wa dini katika maendeleo ya Taifa na kuwataka waumini hao waendelee kuifanya kazi nzuri wanayoifanya katika jamii.

Mhe. Mtambi amewataka kuwahamasisha wazazi na walezi kukemea mmomonyoko wa maadili katika jamii na kulea familia zao kwa misingi ya utamaduni wa Kitanzania ili kupata Taifa bora kwa hapo baadaye na kuwakemea watu wachache katika jamii wanaotumika kwa kudanganywa na wasioitakia mema Tanzania.

Akijibu maombi ya wanawake hao, Kanali Mtambi amewachangia wanawake hao ng’ombe wawili na Mkuu wa Wilaya ya Musoma Mhe. Juma Chikoka amechangia ng’ombe mmoja kwa ajili ya chakula kwa siku hizo tano wakiwa katika Manispaa ya Musoma.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Musoma Mhe. Juma Chikoka amewakaribisha wanawake hao katika Wilaya ya Musoma na kuwashukuru kwa kuchagua kufanyia kongamano hilo katika Wilaya ya Musoma.

Mhe. Chikoka amewapongeza wanawake hao kwa kujitoa kwako kumtumikia Mungu na kuwapongeza kwa kuwa kongamano lao lilikuwa limefana sana.

Kwa upande wake, Katibu wa Kamati ya Amani na Maridhiano Mkoa wa Mara Shekhe Juma Masiroli ambaye pia alishiriki hafla ya ufunguzi wa kongamano hilo amewapongeza wanawake wa TMRC kwa kuamua kufanya kongamano la kuwafundisha masuala mbalimbali muhimu katika jamii.

Sheikh Masiroli amewataka wanawake kuliombea Taifa na hususan katika kipindi hiki cha uchaguzi, kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kuuombea Mkoa wa Mara na wananchi wake amani. 

Akisoma risala kwa niaba ya wanawake hao Bi. Leah Jacob Rutabija amesema kongamano hilo linawakutanisha wanawake zaidi ya 400 kutoka mikoa yote hapa nchini na linafanyika kuanzia tarehe 11-15 Juni, 2025 katika eneo la Kigera, Manispaa ya Musoma kwa ajili ya kumuenzi Askofu Mstaafu wa Kanisa hilo Askofu Jacob Rutubija aliyekua kiongozi katika Jimbo la Mara.

Bi. Leah amesema Kongamanao la mwaka huu limeambatana na maombi maalum ya kuliombea Taifa nchi inapoekelea uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 pamoja na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Bi. Leah alitoa ombi kwa Mkuu wa Mkoa wa Mara kuwasaidia bajeti ya kongamano hilo ambalo litagharimu milioni 20 kwa siku zote tano na kuongeza kuwa tayari akina mama hao wamepata kiasi cha fedha za kuanzia na wanaendelea kuomba michango kutoka kwa wadau mbalimbali.

Hafla ya uzinduzi ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa kanisa la TMRC na baadhi ya viongozi na maafisa kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Mtambi aipongeza Bunda TC kwa hati safi miaka mitano mfululizo

    June 13, 2025
  • Mtambi aitaka Bunda DC kuwasilisha Mkakati wa kukusanya milioni 700

    June 13, 2025
  • Mtambi aipongeza Halmashauri ya Rorya

    June 12, 2025
  • Mtambi awataka wanawake kugombea nafasi za uongozi

    June 12, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa