• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi awataka wananchi kushiriki uchaguzi wa Serikali za Mitaa

Posted on: September 23rd, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo ofisini kwake amezungumza na Waandishi wa Habari kuhusu maandalizi ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2024 katika Mkoa wa Mara na kuwataka wananchi kujitokeza kwa wingi kujiandikisha ili waweze kushiriki uchaguzi huo.

Mhe. Mtambi amesema “kuanzia tarehe 11 hadi 20 Oktoba, 2024 kila mwananchi ajitokeze kujiandikisha kwenye daftari la mpiga kura ili apate haki ya kupiga na kupigiwa kura kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa, na mtu asipojiandikisha hataweza kupiga kura katika uchaguzi huo”.

Mhe. Mtambi amesema tarehe 15 Agosti, 2024 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Mohamed Mchengerwa alitoa tangazo la uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa mwaka 2024 na kueleza kuwa utafanyika tarehe 27 Novemba, 2024.

Mhe. Mtambi amesema katika kuelekeza uchaguzi wa Serikali za Mitaa yapo matukio muhimu ambayo ni pamoja na maelezo kuhusu uchaguzi wa Serikali za Mitaa ambayo yatatolewa rasmi tarehe 26 Septemba, 2024 na wasimamizi wa uchaguzi katika maeneo yao ya utawala na uandikishaji wa wapiga kura litakalofanyika kwa siku kumi kuanzia tarehe 11-20 Oktoba, 2024.

Mhe. Mtambi amesema kuwa kila mwananchi anapaswa kujiandikisha katika Kijiji, Mtaa au Kitongoji chake kwenye kituo ambacho atapigia kura, na vituo hivyo vitaainishwa na wasimamizi wa uchaguzi katika maeneo hayo.

Mhe. Mtambi amezitaja sifa za mwananchi anayepaswa kujiandikisha kuwa ni pamoja na awe raia wa Tanzania mwenye umri wa miaka 18 au zaidi, awe ni mkazi wa maa, kijiji au kitongoji ambapo uchaguzi unafanyika.

Kanali Mtambi amesema zoezi la kuchukua na kurejesha fomu kwa wanaogombea nafasi za uongozi ni tarehe 01 hadi 07 Novemba, 2024 na zoezi la uteuzi wa wagombea litafanyika tarehe 8 Novemba, 2024 na kuwataka wananchi kujitokeza kugombea nafasi mbalimbali zinazogombaniwa katika uchaguzi huo.

Amezitaja nafasi hizo kuwa ni Mwenyekiti wa Mtaa, wajumbe wa kamati ya mtaa kwa halmashauri za miji na Manispaa; Mwenyekiti wa Kijiji, wenyeviti wa vitongoji na wajumbe wa Halmashauri ya Kijiji kwa Halmashauri za Wilaya.

Mhe. Mtambi amesema kampeni kwa ajili ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa zitafanyika tarehe 20-26 Novemba, 2024 baada ya vyama vya siasa kuwasilisha ratiba ya kampeni zao kwa Kamanda wa Polisi wa Wilaya tarehe 14 Novemba, 2024 kwa mujibu wa mwongozo wa ratiba za uchaguzi.

Kanali Mtambi amevitaka vyama vya siasa kutoa ushirikiano kwa wasimamizi wa uchaguzi na viongozi wa Serikali waliopo katika maeneo yao na kuzingatia ratiba ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa mwaka 2024 ili uchaguzi ufanyike kwa mujibu wa miongozo, sheria na kanuni.

Akitoa ufafanuzi kuhusiana na uandikishaji, Mhe. Mtambi amesema katika Mkoa wa Mara kulikuwa na zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Mpiga Kura lililofanyika kuanzia tarehe 4 -10 Septemba, 2024, zoezi hilo halihusiani na uandikishaji wa wapiga kura kwa ajili ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024.

Kauli mbiu ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa mwaka 2024 ni “Serikali za Mitaa, Sauti ya Wananchi, Jitokeze Kushiriki Uchaguzi”.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa