• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi awataka wananchi kujifunza kilimo mseto

Posted on: November 16th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo amefunga maonesho ya tisa ya kilimo mseto yaliyokuwa yanaendelea katika Kituo cha Mafunzo ya Kilimo Mseto katika eneo la Bweri, Manispaa ya Musoma na kuwataka wananchi kuendelea kukitumia kituo hicho kujifunza kilimo mseto.

Akizungumza wakati wa hafla ya kufunga maonesho hayo, Mhe. Mtambi amesema kuwa kituo hicho ambacho kinamilikiwa na Shirika la Vi Agroforestry ni sehemu muhimu kwa wananchi wa Mkoa wa Mara kwenda kujifunza mambo mbalimbali kuhusu kilimo mseto ili kuweza kubadilisha maisha yao.

“Hapa ni sehemu muhimu sana kwa wananchi kuja kujifunza na kubadilishana mawazo kuhusu kilimo mseto na kupata ushauri kutoka kwa wataalamu na wazoefu wa kilimo mseto” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amelipongeza shirika la Vi Agroforestry na washirika wake kwa kuandaa maonesho hayo kila mwaka na kukifungua kituo hicho wakati wote ili wananchi waweze kwenda wakati wowote kujifunza kilimo mseto.

Mkuu wa Mkoa amezitaka Halmashauri za Mkoa wa Mara kuwapeleka wanafunzi kwa nyakati tofauti tofauti wa shule za msingi na sekondari zote za Mkoa wa Mara katika kituo hicho ili eneo hilo liwe linatembelewa wakati wote na watu wanaopenda kujifunza kuhusu kilimo mseto.

Wakati huo huo, Mhe. Mtambi amewataka wananchi waliohudhuria maonesho hayo kushiriki uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika hapa nchini tarehe 27 Novemba, 2024 hapa nchini na kuongeza kuwa kilimo mseto bila viongozi bora na wapenda maendeleo hamna maendeleo.

Kauli mbiu ya maonesho hayo kwa mwaka huu ni Kilimo Mseto kwa Mifumo Endelevu ya Chakula na yalifunguliwa rasmi tarehe 14 Novemba, 2024 na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Dustan Kitandula.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Rorya Mhe. Dkt. Khalfan Haule ameipongeza Vi Agroforestry kwa kazi nzuri wanayoifanya katika kituo hicho kuhusu kilimo mseto na kuwahamasisha wananchi kukitumia kituo hicho vizuri kujifunza na kuyafanyia kazi mafunzo hayo.

Aidha, Dkt. Haule amependekeza Wakala za Barabara kupanda miti pembezoni mwa barabara ambayo itakuwa ikitunzwa na wamiliki wa maeneo yanayopakana na barabara hizo ili kuongeza idadi ya miti inayopandwa hapa nchini.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Musoma Mhe. Juma Chikoka amesema maonesho hayo yamefanyika kwa siku tatu na kwa muda huo wananchi wamejifunza namna bora ya kutumia eneo dogo kupata mavuno mengi.

Mhe. Chikoka amewataka wananchi wa Wilaya ya Musoma kutenga muda na kuja kujifunza katika kituo hicho na kuitumia elimu watakayoipata katika mashamba yao na kubadilisha maisha yao.  

Akiwa katika maonesho hayo, Mkuu wa Mkoa alipata nafasi ya kutembelea vipando, mabanda na kutoa zawadi kwa  washindi mbalimbali waliofanya vizuri zikiwemo Halmashauri, taasisi, vikundi na shule za msingi na sekondari

Hafla ya kufunga maonesho hayo imehudhuriwa na Wakuu wa Wilaya za Mkoa wa Mara, Sekretarieti ya Mkoa wa Mara, Wakurugenzi wa Halmashauri, wataalamu wa kilimo, mifugo, uvuvi na kilimo mseto, na wananchi kutoka mikoa mbalimbali.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa