• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi awapongeza wanamara kwa ukomavu wa kisiasa

Posted on: November 27th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo amepiga kura kuwachagua viongozi wa Serikali ya Mtaa katika kituo kilichopo Ofisi ya Kata Mukendo, Manispaa ya Musoma na kuwapongeza wananchi wa Mkoa wa Mara kwa ukomavu wa kisiasa na kuwataka wajitokeze kwa wingi kupiga kura.

Akizungumza mara baada ya kupiga kura Mhe. Mtambi amesema katika kampeni za uchaguzi wa Serikali za Mitaa wananchi wameonyesha ukomavu wa kisiasa uliosababisha kampeni kufanyika kwa amani na utulivu na hamna malalamiko ya vyama au wagombea kufanyiwa fujo wakati wa kampeni.

“Ninawapongeza wananchi wa Mkoa wa Mara kwa ukomavu mkubwa wa kisiasa waliouonyesha katika kipindi chote cha kampeni na ninawakumbusha kujitokeza kwa wingi kupiga kura ili kuwachagua viongozi wanaowataka” amesema Mhe. Mtambi.

Kanali Mtambi amevitaka vyama vya siasa na wanachama wao kuheshimu na kuzifuata kanuni za uchaguzi wa Serikali za Mitaa ambazo walishiriki kuzitunga na kama kuna malalamiko yoyote wanaweza kuwasilisha malalamiko hayo sehemu zinazohusika kwa mujibu wa kanuni za uchaguzi.

Aidha, Mkuu wa Mkoa amepiga marufuku mikusanyiko isiyo ya lazima wakati huu wa uchaguzi na kuwataka wananchi kuhakikisha kuwa baada ya kupiga kura wanaenda kuendelea na shughuli zao za kila siku.

Mhe. Mtambi amewaonya watu wanaopanga kufanya vurugu na kuahidi kuwa Kamati ya Usalama ya Mkoa wa Mara na wananchi wa Mkoa wa Mara hawatamvumilia mtu yoyote atakayeanzisha fujo katika kipindi hiki na kuwahakikishia wananchi kuwa Serikali itawachukulia hatua za kisheria watu wote wanaoanzisha vurugu wakati huu.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Musoma Mhe. Juma Chikoka akizungumza katika eneo hilo amewaomba wananchi wa Wilaya ya Musoma kujitokeza kwa wingi kushiriki uchaguzi na kuwahakikishia usalama wao wakati wote wa uchaguzi.

Mhe. Chikoka pia amewataka wananchi kuachana na mikusanyiko isiyo ya lazima na kutoa taarifa kwa viongozi wanapohisi kuna uwezekano wa uvunjifu wa amani katika maeneo yao.

Vituo vya kupigia kura vimefunguliwa saa mbili kamili asubuhi na vinategemewa kufungwa saa 10 jioni na baada ya kupiga kura wananchi wanashauriwa kuondoka katika eneo la kituo cha kupiga kura kwa utulivu na amani.

Leo ni siku ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa ambapo wananchi wanachagua viongozi mbalimbali wakiwemo wenyeviti wa Mitaa/Vijiji, wajumbe wa serikali ya mtaa/kijijji, wenyeviti wa vitongoji na kauli mbiu ya mwaka huu ni Serikali za Mitaa, Sauti ya Wananchi, Jitokeze kushiriki Uchaguzi.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa