• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi avitaka vyama vya siasa kuzingatia kanuni za uchaguzi

Posted on: November 28th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Evans Alfred Mtambi leo ameshiriki mazishi ya watu nane waliofariki katika mafuriko Mjini Tarime na kuwataka viongozi wa vyama vya siasa kuzingatia kanuni za uchaguzi wa Serikali za Mitaa katika kutoa malalamiko kuhusiana na uchaguzi uliofanyika hapa nchini tarehe 27 Novemba, 2024.

Mhe. Mtambi amesema vyama vya siasa vyote 19 vilivyoshiriki uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2024 vilishiriki kutunga kanuni za uchaguzi ambazo ndio zinaongoza shughuli zote za uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa sasa. 

“Mchakato wa uchaguzi bado unaendelea, kanuni za uchaguzi zimeainisha nini cha kufanya katika kila hatua ya uchaguzi, kwa mujibu wa kanuni hizo kama kuna chama kina malalamiko yanapaswa kuwasilishwa rasmi kwa wasimamizi wa uchaguzi ndani ya siku 30 na yatasikilizwa” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amevihakikishia vyama vya siasa kuwa Mkoa wa Mara katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaongozwa na kanuni za uchaguzi kwenye kushughulikia masuala yote ya uchaguzi na kuwataka viongozi wa vyama vya siasa kama wanamalalamiko kufuata taratibu zilizowekwa katika kanuni za uchaguzi.

Aidha, amevipongeza vyama vya siasa, wanasiasa na wananchi wa Mkoa wa Mara kwa ukomavu wa kisiasa waliouonyesha wakati wote wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na kuwataka kuendeleza amani na utulivu uliopo.

“Katika uchaguzi huu, hamna aliyeshindwa wala aliyeshinda ila wanamara kwa umoja wetu ndio tumeshinda, uchaguzi umepita sasa tuendelee kuishi kama ndugu na kushikamana kama Watanzania bila kujali tofauti za itikadi zetu” amesema Mhe. Mtambi.

 Kanali Mtambi amesema viongozi wateule waliochaguliwa bado hawajaapishwa ili kuendelea na majukumu yao na wataapishwa kwa mujibu wa kanuni za uchaguzi zinavyoelekeza ili waweze kuanza kutekeleza majukumu yao katika jamii.

Kwa upande wake, Mbunge wa Tarime Mjini Mhe. Michael Kembaki amewashukuru wananchi Wilaya ya Tarime kwa ushiriki wao katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2024 na kufanya uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa amani na usalama.

Mhe. Kembaki amewashukuru sana wananchi kwa namna walivyotoa ushirikiano katika kipindi chote cha uchaguzi ikiwa ni pamoja na kushiriki kampeni za uchaguzi na baadhi yao kugombea nafasi mbalimbali zilizokuwa zinagombaniwa.

Mhe. Kembaki ametoa pole kwa wafiwa na wote walioathirika na mafuriko hayo na kuipongeza Serikali na Vyombo vya Usalama kwa namna walivyoshiriki katika maafa hayo tangu mafuriko yalipotokea.

Mafuriko makubwa yalitokea kandokando ya Mto Mori katika Kata ya Nyamisangula, Mji wa Tarime na  kusomba nyumba nne na watu tisa kupoteza maisha huku watu wawili wakinusurika kifo na madaraja mawili yakiathirika katika eneo hilo tarehe 24 Novemba, 2024.

Mazishi hayo yamehudhuriwa pia na Kamati ya Usalama Mkoa wa Mara, Kamati ya Usalama Wilaya ya Tarime, viongozi wa Chama cha Mapinduzi wakiongozwa na Mwenyekiti wa Mkoa wa Mara Mhe. Patrick Chandi, Watumishi wa Sekretarieti ya Mkoa wa Mara, viongozi na watumishi wa Halmashauri ya Mji wa Tarime.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Mwenge wa Uhuru kupitia miradi ya bilioni 26.6 Mara

    August 13, 2025
  • Miradi ya TACTIC kuboresha muonekano wa Musoma

    August 12, 2025
  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa