• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi avitaka vyama vya siasa kufanya kampeni za kiustaarabu

Posted on: November 12th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo ameongoza kikao kazi kati ya Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (TAKUKURU) na viongozi wa vyama vya Siasa Mkoa wa Mara kilichofanyika katika Ukumbi wa Uwekezaji na kuwataka kufanya kampeni za uchaguzi wa Serikali za Mitaa kiustaarabu.

Akizungumza katika kikao hicho, Mhe. Mtambi amevitaka vyama vya siasa kufanya kampeni za kiustaarabu na kuhakikisha kuwa siasa za maji taka, mifarakano, ukabila na kujenga chuki zisiwe Sehemu ya Mkoa wa Mara.

“Kamati ya Usalama ya Mkoa tumejipanga kuhakikisha kuwa uchaguzi unafanyika kwa amani na utulivu na mtu yeyote anayejipanga kuharibu uchaguzi kwa namna yoyote ile atachukuliwa hatua kali za kisheria” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amewataka viongozi wa vyama vya siasa kuwahamasisha wananchi wa Mkoa wa Mara kujitokeza kwa wingi kwenda kupiga kura tarehe 27 Novemba, 2024 ili kutumia haki yao ya kikatiba ya kuchagua na kuchaguliwa kuwa viongozi bora watakaowaletea maendeleo yao.

Kanali Mtambi amesema wananchi wa Mkoa wa Mara ni wasikivu ni wastaarabu na wanautulivu wa kisiasa na amewataka wananchi wa Mkoa wa Mara wasitumike na wanasiasa uchwara wanaotaka kuwatumia kuharibu uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Mhe. Mtambi amevitaka vyama vya siasa vinavyoshiriki uchaguzi wa Serikali za Mitaa vitakavyoshindwa katika uchaguzi huu kurudi na kujipanga upya ili kuweza kupanga mipango mizuri ya kushinda katika chaguzi zijazo.

 Kwa upande wake, Kamanda wa TAKUKURU Mkoa wa Mara Mohamed Sharif akitoa mada kwenye kikao hicho ameviomba vyama vya siasa kutoa ushirikiano kwa TAKUKURU kwa kutoa taarifa wanapobaini matukio yanayohisiwa kuwa ya rushwa.

“Kwa ushirikiano wetu tukiamua kwa pamoja kuna kuwa hamna rushwa au inaweza kuzuiwa kwa kiasi kikubwa amesema Bwana Sharif na kuwataka viongozi hao kuwapa elimu wanachama na viongozi wao ili kuweza kuizuia rushwa ndani nan je ya vyama vyao.  

Bwana Sharif ameeleza kuwa malengo makubwa ya taasisi hiyo ni kuchochea maendeleo ya utawala bora na kuzuia na kupambana na rushwa hapa nchini na kuongeza kuwa kutokana na malengo hayo, taasisi hiyo inahusika na kufuatilia mwenendo mzima wa uchaguzi.

Bwana Sharif ameeleza kuwa wakati wa uchaguzi wananchi wanatakiwa kutumia fursa hiyo kutafakari changamoto zinazowakabili katika maeneo yao ili waweze kujua namna ya kuzitatua na kumtafuta mtu atakayewaongoza katika kuleta maendeleo yao.  

Bwana Sharif amesema katika utafiti wa TAKUKURU katika changuzi za mwaka 2014, 2019 na 2020 umebaini kuwa wakati wa uchaguzi kunakuwepo na matatizo ya kimaadili ambapo kuna kuwa na matukio ya rushwa, kampeni kabla ya ratiba rasmi ya kampeni, lugha za matusi, kejeli na kashfa na tatizo la vyama kuingilia kampeni za vyama vingine vya siasa.

Bwana Sharif amebainisha kuwa TAKUKURU imebaini viashiria mbalimbali vya rushwa na mianya ambayo inatumika katika kutoa na kupokea rushwa nyakati za uchaguzi na taasisi hiyo imejipanga kikamilifu kuweza kufuatilia uchaguzi katika maeneo mbalimbali.

Kamanda wa TAKUKURU amewataka viongozi wa vyama vya siasa kutoa ushirikiano kwa TAKUKURU ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa za matukio yenye viashiria vya rushwa ili TAKUKURU iweze kufuatilia matukio hayo na kutoa elimu kwa viongozi wengine na wanachama wa vyama vyao kuhusiana na masuala ya rushwa katika uchaguzi.

Kikao hicho kimehudhuriwa na viongozi wa vyama vya siasa Mkoa wa Mara, Kamati ya Usalama ya Mkoa wa Mara, Menejimenti ya Sekrearieti ya Mkoa wa Mara na Maafisa kutoa TAKUKURU.  

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa