• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi atoa wiki nane Serengeti kukamillisha nyumba ya mtumishi wa afya

Posted on: October 8th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo ametoa wiki nane kwa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti kukamilisha nyumba ya mtumishi wa afya iliyojengwa katika Zahanati ya Getarungu kwa nguvu za wananchi ili watumishi wa zahanati hiyo waishi jirani na zahanati hiyo.

Mhe. Mtambi ametoa agizo hilo baada ya kupokea taarifa kuhusu Halmashauri kutokutekeleza agizo lililotolewa mapema mwaka huu na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara wakati huo Mhe. Said Mohammed Mtanda alipofanya ziara katika zahanati hiyo Machi, 2024.

“Ninataka ndani ya hizo wiki nane nyumba hii iwe inatumika, haiwezekani tumejengewa zahanati nzuri namna hii na Halmashauri inashindwa kukamilisha nyumba iliyojengwa kwa nguvu za wananchi” amesema Mhe. Mtambi.

Kanali Mtambi amemtaka Mkuu wa Wilaya ya Seregeti kusimamia agizo hilo na kuhakikisha Mganga wa Kituo hicho anaishi hapo katika muda huo ili wananchi waweze kupata huduma na hususan wakati wa usiku na kuwaahidi wananchi kuwa baada ya wiki nane ataenda kukagua.

Mhe. Mtambi amewapongeza wananchi wa Kijiji cha Getarungu kwa kujitolea kujenga nyumba hiyo kwa ajili ya mtumishi wa afya ili waweze kupata huduma za afya.

Aidha, amewataka wananchi kushiriki kikamilifu uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa mwaka 2024 na uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 na kuhakikisha wanachagua viongozi bora.

Akizungumza katika mkutano huo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Boniface Simbachawene amewataka wananchi kuitunza Hifadhi ya Taifa ya Serengeti (SENAPA) ili waendelee kupata miradi ya maendeleo kutoka kwa wafadhili.

Akizungumza baada ya kuzindua zahanati hiyo, Mhe Simbachawene amesema zahanati hiyo ambayo ni sehemu ya zahanati nane zilizojengwa na Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) kwa ufadhili wa Benki ya Maendeleo ya Ujerumani (KFW) kwa gaharama ya shilingi milioni 387 kila mmoja.

“Manufa haya tunayapata kwa sasa watu wa Getarungu ni wahifadhi wazuri na ndio maana mmefanikiwa kupata mradi huu mkubwa wa zahanati” amesema Mhe. Simbachawene.

Mhe. Simbachawene ameipongeza TANAPA na KFW kwa usimamizi mzuri wa mradi huo, gharama ya mradi inaonekana kupitia mradi huo.

Aidha, Mhe. Simbachawene amewaahidi wananchi kujenga daraja linalounganisha vitongoji wa kijiji hicho ili kuwawezesha wananchi kupata mawasiliano wakati wote na hususan wakati wa masika ambapo mto unaotenganisha vitongoji hivyo ukijaa wananchi wanashindwa kuvuka.

Akiwa katika Wilaya ya Serengeti pia Mhe. Simbachawene ameweka jiwe la msingi katika mradi wa barabara mpya ya stendi mpya- Koreri katika Mji wa Mugumu yenye kilomita nane na madaraja 10 na mitaro yenye thamani ya shilingi milioni 499 inayosimamiwa na Wakala wa Barabara za Vijijini (TARURA)

Akizungumza katika eneo hilo, Mhe. Simbachawene ameipongeza TARURA katika utekelezaji mzuri wa mradi huo na kusema kuwa baada ya kukagua na kupokea taarifa ya mradi huo ameiona thamani ya fedha iliyotumika kwenye barabara hiyo.

 Ziara hiyo imehudhuriwa na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Mara Mhe. Patrick Chandi Marwa, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Gerald Musabila Kusaya, Kamati ya Usalama ya Mkoa na Wilaya ya Serengeti, viongozi wa Halmashauri na watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti.

Ziara ya Mhe. Simbachawene imehitimishwa katika Wilaya ya Bunda baada ya kukagua miradi na kufanya mkutano wa hadhara katika eneo la stendi ya zamani tarehe 4 Oktoba, 2024. 

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Mtambi aipongeza Bunda TC kwa hati safi miaka mitano mfululizo

    June 13, 2025
  • Mtambi aitaka Bunda DC kuwasilisha Mkakati wa kukusanya milioni 700

    June 13, 2025
  • Mtambi aipongeza Halmashauri ya Rorya

    June 12, 2025
  • Mtambi awataka wanawake kugombea nafasi za uongozi

    June 12, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa