• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi ataka wakandarasi wazawa kujiongeza

Posted on: April 13th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Evans Alfred Mtambi leo ametembelea ujenzi wa Barabara ya Mogabiri- Nyamongo (Km 25) inayojengwa na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) na kuwataka wakandarasi wazawa kujiongeza kwa kuboresha utendaji wao ili waweze kushindana katika zabuni za kimataifa.

Mhe. Mtambi amesema wakandarasi wazawa wanauwezo mkubwa wa kufanyakazi mbalimbali na hata kugombea zabuni za kimataifa kama watakuwa makini katika utendaji wao wanapotekeleza miradi wanayopewa.

“Mkiacha tabia ya kukimbilia kuongeza wake na kufanya starehe baada ya kupata malipo ya kutekeleza miradi vizuri mtafanikiwa na mtafika mbali katika kushindania zabuni na kutekeleza miradi” amesema Mhe. Mtambi.

Akizungumzia kuhusu barabara hiyo, Mhe. Mtambi amesema amekagua na kuridhishwa na kazi inayoendelea katika utekelezaji wa mradi huo na kumtaka mkandarasi kukamilisha barabara hiyo kwa mujibu wa mkataba.

“Hii ni barabara muhimu sana kwa uchumi wa Mkoa wa Mara na inaunganisha Wilaya za Tarime na Serengeti na inawaunganisha watalii wanaopitia nchi ya Kenya kuingia katika Hifadhi ya Serengeti kiurahisi zaidi” amesema Mhe. Mtambi.

Aidha, amesema barabara hiyo ni muhimu kwa kusafirisha mazao ya kilimo na wananchi kiurahisi kwenda katika maeneo mbalimbali na kuwataka wananchi wa Mkoa wa Mara kumshukuru Mhe. Rais kwa kufanikisha mradi huo na kusaidia katika kuutunza ili udumu muda mrefu.

Mhe. Mtambi amesema kuna baadhi ya Wilaya ambazo makao makuu yake hayajaunganishwa na lami katika Mkoa wa Mara lakini Mhe. Rais baada ya kuliona hilo ameanzisha miradi mbalimbali ambayo itasaidia kuondoa tatizo hilo.

Wakati huo huo, Mhe. Mtambi amekemea wazabuni na wakandarasi waliopewa zabuni na wanaokwamisha utekelezaji wa miradi katika Mkoa wa Mara na kuwatahadharisha kuwa Mkoa utachukua hatua stahiki kuhakikisha hawapati tena zabuni katika Mkoa wa Mara.

“Kama mzabuni au mkandarasi unajiona huna uwezo wa kuleta vifaa na kutekeleza mradi usiombe zabuni katika Mkoa wa Mara, tutakuchukulia hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kuwablacklist wasifanye kazi katika Mkoa wa Mara” amesema Mhe. Mtambi.

Kwa upande wake, Meneja wa TANROADS Mkoa wa Mara Mhandisi Vedastus Maribe amesema utekelezaji wa barabara hiyo upo katika nzuri na tayari mkandarasi ameshajenga madaraja makubwa saba na madaraja madogo zaidi ya 30 na barabara yenye urefu wa kilometa sita imekamilika na imeanza kutumika.

“Utekelezaji wa mradi huu upo katika asilimia 56 na unatarajiwa kukamilika mwaka huu kwa mujibu wa mkataba” amesema Mhandisi Maribe.

Akizungumzia kuhusu barabara nyingine zinazoendelea kujengwa katika Mkoa wa Mara, Mhandisi Maribe amesema kwa sasa kuna miradi ya barabara mitatu ya barabara za kuelekea Mji wa Mugumu  inayoendelea kujengwa ikiwa katika hatua mbalimbali.

Mhandisi Maribe amesema ujenzi wa barabara za Musoma- Busekela katika eneo la Kusenyi- Musoma (km 40) na barabara ya Utegi -Shirati (km 27) upo katika hatua za zabuni ya kuwapata wakandarasi.

Kwa upande wake, Mama Monica Charles Josia Mkazi wa Kijiji cha Komerele amemshukuru Mhe. Rais kwa kujenga barabara hiyo na kuongeza kuwa imewaondolea adha ya usafiri na kwa sasa wanapata usafiri kwa bei nafuu.

“Zamani tulikuwa tunaenda Tarime Mjini kwa shilingi 10,000 na kurudi inakuwa shilingi 20,000 lakini sasa nauli imekuwa ni shilingi 2,000 tu kwenda na kurudi inakuwa 4,000; hatukuwahi kulipa nauli ndogo kiasi hiki” amesema Mama Josia.

Mama Josia amemshukuru pia Mbunge wa Jimbo la Tarime Vijijini Mhe. Mwita Waitara kwa ufuatiliaji wake wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika jimbo hilo na Mkoa wa Mara kwa usimamizi mzuri wa mradi huo.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Mtambi aipongeza Bunda TC kwa hati safi miaka mitano mfululizo

    June 13, 2025
  • Mtambi aitaka Bunda DC kuwasilisha Mkakati wa kukusanya milioni 700

    June 13, 2025
  • Mtambi aipongeza Halmashauri ya Rorya

    June 12, 2025
  • Mtambi awataka wanawake kugombea nafasi za uongozi

    June 12, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa