• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MTAMBI ATAKA HAMASA UCHANGIAJI CHAKULA SHULENI

Posted on: January 24th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo ameongoza kikao cha tathmini ya utekelezaji wa Mkataba wa Lishe ngazi ya Mkoa kwa kipindi cha Julai- Desemba kwa mwaka 2024/2025 na kuzitaka Halmashauri kuongeza uhamasishaji katika masuala ya uchangiaji wa chakula ili wanafunzi wote wa Mkoa wa Mara waweze kupata chakula shuleni.

Akizungumza katika kikao hicho, Mhe. Mtambi amesema Halmashauri hazijafanya uhamasishaji wa kutosha kuhusu uchangiaji wa chakula kwa hiari na haziwatumiaa wadau mbalimbali waliomo katika Halmashauri zao wakiwemo viongozi wa dini, viongozi wa kimila na mashirika yasiyo ya kiserikali.

“Tangu nimekuja Mkoa wa Mara nimeona mkutano mkubwa mmoja tu kuhusiana na masuala ya ulishaji chakula shuleni na ambao uliandaliwa na ofisi yangu, lakini Halmashauri sijaona inafanya jambo kubwa kuhusiana na uhamasishaji wa kuchangia chakula shuleni” amesema Mhe. Mtambi.  

Mhe. Mtambi amesema wakati wa kikao cha tathmini ya kitaifa Agosti, 2024 Mkoa wa Mara ulikuwa ni miungoni mwa mikoa 11 iliyofanya vibaya ya utoaji wa chakula mashuleni jambo ambalo halikubaliki wakati Mkoa wa Mara ndio ulikuwa wakwanza kufanyiwa majaribio na mwongozo wa Kitaifa wa utoaji wa chakula shuleni umetayarishwa Mara.

“Mimi niliambiwa mikoa ambayo awali ilikuja kujifunza Mara kutoa chakula shuleni inafanya vizuri kuliko Mkoa wa Mara ambao ulikuwa wakwanza kitaifa na ulishiriki kuandaa mwongozo wa utoaji wa chakula kwa wanafunzi, hilo halikubaliki, tubadilike” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amezitaka Halmashauri zote kutunga sheria ndogo ndogo za kuwabana wazazi na walezi wa wanafunzi kuchangia chakula mashuleni ili wasipochangia kwa hiari wabanwe kuchangia ili watoto wapate chakula wakiwa shuleni.

Mhe. Mtambi amewataka viongozi, wasimamizi wa elimu na watendaji kwa ujumla kuhakikisha wanafunzi wote wanapata chakula angalau mara moja shuleni na kuhakikisha uchangiaji kwa kupitia wazazi, walezi na wadau unafanyika.

Kwa upande wake, Afisa Lishe wa Mkoa wa Mara Bibi Grace Martin amesema shule nyingi zinatoa huduma ya chakula shuleni hata hivyo idadi ya wanafunzi wanaopata shuleni bado ipo kidogo kwa sababu sio watoto wote wanaopata chakula shuleni.

Bibi Martin amesema kutokana na uchangiaji wa wazazi na walezi na sababu nyingine shule nyingi zinatoa huduma za chakula kwa wananfunzi wachache jambo ambalo ni kinyume na miongozo ya Serikali kuhusu utoaji wa chakula shuleni.

Bibi Martin amesema kwa sasa Mkoa wa Mara una wastani wa asilimia 68 ya utoaji wa chakula shuleni na Halmashauri ya Tarime TC imefanya vizuri katika uchangiaji wa chakula shuleni.

 Kikao hicho kimehudhuriwa na Katibu Tawala Mkoa wa Mara Bwana Gerald Kusaya, Wakuu wa Wilaya na Makatibu Tawala wa Wilaya, Menejimenti ya Sekretarieti ya Mkoa, Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa, Timu ya Usimamizi wa Sekta ya Afya Mkoa, Waganga Wakuu, Maafisa Lishe, Waweka Hazina, Maafisa Utumishi, Maafisa Elimu Msingi na Sekondari na Maafisa Mipango wa Halmashauri zote za Mkoa wa Mara.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa