• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi asistiza agizo lake kuhusu madawati Tarime DC

Posted on: March 5th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo ameongoza kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) na kukumbushia agizo lake la kushikiria posho za viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime mpaka madawati yaliyotengewa fedha yawe yamewafikia wanafunzi.

Mhe. Mtambi alitoa agizo hilo tarehe 26 Februari, 2025 akiwa katika ziara ya kawaida Halmashauri ya Wilaya ya Tarime na leo kulirudia tena katika kikao cha RCC wakati wa majadiliano ya mipango na bajeti ya mwaka wa fedha 2025/2026

“Kama madawati hayo hayatapelekwa shuleni kwa wakati hata mimi posho yangu nikija Tarime msinipe mpaka wanafunzi watakapopata madawati” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi ameutaka Mgodi wa North Mara kumpatia taarifa za maendeleo ya utengenezaji wa madawati hayo ili aweze kujua nani anayekwamisha utengenezaji wa madawati hayo na kuwafanya wanafunzi kukosa madawati huku fedha zikiwa zimetengwa kwa muda mrefu bila kununua madawati hayo.

Mhe. Mtambi amewataka wananchi wa Mkoa wa Mara kufuatilia zabuni zinazotangazwa na Mgodi wa Dhahabu wa North Mara ili waweze kunufaika na utekelezaji wa miradi ya CSR katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime.

Mhe. Mtambi amewataka wazabuni watakaopata zabuni za kutekeleza miradi hiyo kwa wakati ili wananchi waweze kunufaika na huduma zitakazotolewa na miradi hiyo.

Kwa upande wake, Mwakilishi wa Meneja Mkuu wa Mgodi wa North Mara Bwana Hermence Christopher amesema utekelezaji wa miradi ya CSR katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime imechelewa kutokana na taratibu mpya za manunuzi ndani ya mgodi.

Bwana Christopher amesema taratibu zinautaka mgodi kwenye manunuzi yote makubwa kupata kibali Tume ya Madini na manunuzi ya miradi ya CSR yalikuwa ni ya shilingi zaidi ya bilioni tisa hivyo taratibu za kisheria ilibidi zifuatwe na hivyo kuchelewesha manunuzi.

“Kwa sasa kibali kimepatikana na matangazo zabuni yameshasambazwa ili kuwapata wazabuni watakaotekeleza miradi hiyo ikiwemo utengenezaji wa madawati kwa ajili ya wanafunzi wa Shule za Halmashauri ya Wilaya ya Tarime” amesema Bwana Christopher.

Bwana Christopher amesema wanategemea kutoa kazi ya kutengeneza madawati kwa wazabuni wengi na wanategemea kuanza kutengeneza madawati wiki ijayo na yatakuwa yakisambazwa kwa kadiri yanavyokamilika.

Bwana Christopher amekihakikishia kikao hicho kuwa Mgodi huo unategemea mpaka tarehe 31 Machi, 2025 madawati yatakuwa yametengenezwa na kusambazwa katika shule zenye upungufu wa madawati katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa