• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi akemea ukabila Makundusi

Posted on: April 15th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo tarehe 14 Aprili, 2025 amefanya mkutano wa hadhara na wananchi wa Wilaya ya Serengeti katika Kijiji cha Makundusi, Wilaya ya Serengeti na kukemea vitendo vya ukabila miungoni mwa viongozi na wananchi.

Mhe. Mtambi amekemea vitendo hivyo baada ya kusikiliza kero za wananchi na katika mkutano wa hadhara baada ya kupokea baadhi ya kero zinazozungumzia utengano wa viongozi na wananchi kwa kufuatana na ukabila katika eneo hilo.

“Ndugu zangu ninaomba tubadilike, katika kikao chetu hapa yamejitokeza mambo yanayohusu ukabila, niwaambie tu ukabila haujengi wala hauna manufaa yoyote kwa maendeleo yenu. Tuwakemee wote wanaoendekeza ukabila hata kama ni viongozi wetu” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amewataka wananchi kupendana na kusaidia ili kuishi kwa amani na utulivu na kuacha tabia za kujichukulia sheria mkononi, mila potofu na vitendo visivyofaa katika jamii ambavyo amesema vitarudisha nyuma maendeleo yao.

Mhe. Mtambi amewataka wananchi kuukata ukabila kwa sababu hauna mwisho mzuri na kutanguliza Utanzania wao na kwa kufanya hivyo wanaweza kujifunza na kuishi kwa amani kwa watu wa makabila mengine na kujiletea maendeleo yao na familia zao.

Kanali Mtambi amesema nchi inapoelekea katika uchaguzi, wananchi wawaogope viongozi wanaowagawa kutokana na makabila yao bali wawachague viongozi wanaowaunganisha na kupigania maendeleo ya wananchi wote.

Mhe. Mtambi amewataka wananchi kushiriki uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 na kuwachagua viongozi wanaopenda maendeleo na kuachana na wanaofanya siasa za uchochezi, ukabila na ugombanishi.

Wakati huo huo, Mkuu wa Mkoa wa Mara amesikiliza kero, changamoto na ushauri kutoka kwa wananchi na kutoa maelekezo mbalimbali kutatua kero na changamoto za wananchi wa eneo la Makundusi.

Aidha, ili kutatua kero hizo, Mhe. Mtambi ametoa maagizo mbalimbali kwa Mkuu wa Wilaya ya Serengeti, Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti, Kijiji cha Makundusi na taasisi za Grumeti, RUWASA na kadhalika.  

Mkutano huo ulihudhuriwa pia na Kamati ya Usalama ya Mkoa na Wilaya ya Serengeti, Maafisa kutoka Sekretarieti ya Mkoa wa Mara, viongozi na watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti na wawakilishi wa taasisi za umma na binafsi zilizopo Serengeti.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa