• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi aitaka Tarime TC kuongeza juhudi ukusanyaji wa mapato

Posted on: June 11th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo ameshiriki kikao cha Baraza la Madiwani maalum kwa ajili ya kujadili hoja za Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) katika Halmashauri ya Mji wa Tarime na kuitaka Halmashauri hiyo kuongeza jitihada katika ukusanyaji wa mapato ya ndani.

Akizungumza katika kikao hicho, Mhe. Mtambi amesema mwenendo wa makusanyo ya mapato ya ndani katika Halmashauri hiyo hauridhishi na kuongeza kuwa hadi kufikia tarehe 30 Mei, 2025 Halmashauri hiyo ilikuwa imekusanya asilimia 73 tu ya mapato yaliyotarajiwa kukusanywa katika mwaka wa fedha 2024/2025.

“Ninatoa hadi tarehe 9 Juni, 2025 Halmashauri iwasilishe mkakati utakaoiwezesha kukusanya kwa asilimia 100 mapato ya ndani ifikapo tarehe 30 Juni, 2025” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amesema Halmashauri hiyo imekusanya shilingi bilioni 2.6 tu kati ya shilingi bilioni 3.6 ya lengo la mapato ya ndani na kuitaka Halmashauri hiyo kujipanga vizuri ili kuboresha makusanyo ya Halmashauri.  

Kanali Mtambi pia ameipongeza Halmashauri hiyo kwa kupata hati safi ya ukaguzi kwa miaka mitano mfululizo na kulitaka Baraza la Madiwani kwa kushirikiana na Menejimenti ya Halmashauri hiyo kuibua vyanzo vipya vya mapato ili kusaidia Halmashauri kuweza kujiendesha na kutekeleza miradi ya maendeleo.

Akizungumza katika kikao hicho, Mkuu wa Wilaya ya Tarime Mhe. Meja Edward Gowele amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kupeleka fedha nyingi za kutekeleza miradi ya maendeleo katika Wilaya hiyo.

Meja Gowele amelipongeza Baraza hilo kwa kufanya kazi kwa umoja na ushirikiano na kufanikisha azma yao ya kuwaletea maendeleo wananchi wa Mji wa Tarime na kuongeza kuwa anawaombea kwa Mwenyezi Mungu waweze kuteuliwa tena katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu.

Aidha, amewashukuru kwa ushirikiano wa Baraza la Madiwani kwa ofisi yake, Menejimenti na taasisi nyingine za Serikali katika Wilaya hiyo na kuahidi kuwa maagizo ya Mkuu wa Mkoa wameyachukua kwa utekelezaji na hadi kufikia tarehe 30 Juni, 2025 mapato yatakuwa kwenye wastani mzuri.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Tarime Mhe. Daniel Komote amesema wakati wanaingia Halmashauri ilikuwa na bajeti ndogo sana na fedha zilikuwa zinakusanywa kwa kiasi kidogo chini ya asilimia 80. 

Mhe. Komote amesema kwa sasa Halmashauri imeongeza makusanyo na kwa mwaka huu 2024/2025 walipanga kukusanya shilingi bilioni 3.6 na hadi kufikia tarehe 30 Mei, 2025 walikuwa wamekusanya shilingi bilioni 2.6 ambayo ni sawa na asilimia 73 ya bajeti yao.

“Hii fedha tunategemea kuikusanya ndani ya wiki mbili baada ya wafanyabiashara kulipia gharama za kukodi vibanda katika soko jipya la Tarime lililokamilika na makusanyo yake yalipangwa katika bajeti iliyopo” amesema Mhe. Komote.

Mhe. Komote amesema awali Halmashauri ilikuwa haina mradi mkubwa wa kuimarisha mapato ya ndani ya Halmashauri na baada ya soko la kimkakati kukamilika Halmashauri inategemea kuongeza zaidi ya milioni 500,000 kwa mwaka kutokana na mrdi huu.

Mhe. Komote amesema Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Mji wa Tarime katika kipindi chake cha miaka mitano limeacha alama kubwa kwa kujenga miradi mipya ya kutolewa huduma ya afya, elimu na kadhalika kwa kutumia mapato ya ndani ya Halmashauri.

Kwa upande wake, Mwekahazina wa Halmashauri ya Mji wa Tarime CPA George Adino amesema katika ukaguzi wa mwaka wa fedha 2023/2024 Halmashauri ilikuwa na jumla hoja 70 na baada ya kuwasilisha majibu hoja 36 zimefungwa na 34 zipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji.

CPA Adino mesema kati ya hoja hizo hoja 27 ni mpya na katika hizo hoja 12 zimefungwa na hoja 15 zinaendelea kujibiwa aidha Halmashauri ilikuwa na maagizo matatu kutoka Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) ambayo yapo katika hatua za utekelezaji.

Kikao hicho kilihudhuriwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara, Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Tarime, baadhi ya maafisa kutoka Sekretarieti ya Mkoa wa Mara, Madiwani na Menejimenti ya Halmashauri ya Mji wa Tarime.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa