• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi aitaka FEZA kuwekeza Butiama kumuenzi Mwalimu Nyerere

Posted on: July 25th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo tarehe 25 Julai, 2025 amewapokea na kufanya mazungumzo na viongozi wa Shule za Feza za Jijini Dar es Salaam na kuwahamasisha viongozi hao kujenga Shule ya Feza katika Wilaya ya Butiama.

Akizungumza na viongozi hao, Mhe. Mtambi amesema Butiama ni eneo sahihi la kuwekeza katika masuala ya elimu kwa ajili ya kumuenzi Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na mchango wake katika maendeleo ya elimu ya Tanzania.

“Ninawashauri mjenge Shule hii katika Wilaya ya Butiama, eneo ambalo mazingira yake ni mazuri kwa kujenga taasisi za elimu na ili kumuuenzi Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere na mchango wake katika elimu ya Tanzania” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amezitaja sababu nyingine za kupendekeza Wilaya ya Butiama ni kutokana na uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali kujenga Chuo Kikuu cha Chuo Kikuu cha Mwalimu Julius K. Nyerere cha Kilimo na Teknolojia, Butiama (MJNUAT) ambapo Serikali imewekeza zaidi ya bilioni 102.5 na ujenzi wake upo katika hatua za ukamilishaji.

Aidha, Mhe. Mtambi amesema Mkoa pia umepeleka Shule ya Sekondari ya Amali ya Mkoa wa Mara inayojengwa katika Wilaya na kuongeza kuwa eneo hilo linafikika wakati wote kutokana na uwekezaji wa Uwanja wa Ndege Musoma na Barabara za lami zilizojengwa katika eneo hilo.

Mhe. Mtambi amesema kutokana na uwepo wa Chuo Kikuu cha MJNUAT itakuwa rahisi kwa Shule hiyo kupata wanafunzi watakaosoma katika shule hiyo kutokana na uwepo wa migodi, Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na kuwa jirani na mpaka wa Tanzania na Kenya.   

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Shule za Fedha Bwana Ally Nungu amesema viongozi hao wametembelea mikoa ya Kanda ya Ziwa kuangalia uwezekano wa kujenga Shule ya Feza katika mkoa mmoja kati ya hiyo.  

“Mapendekezo haya yatawasilishwa kwa viongozi na wamiliki wa Shule za Feza na viongozi wa juu wataamua Shule hiyo itajengwa katika Mkoa gani kati ya mikoa ya Kanda ya Ziwa tuliyoitembelea” amesema Bwana Nungu.

Aidha, Bwana Nungu amesema wataitembelea Wilaya ya Butiama na kuona uwezekano wa kuanza mazungumzo kwa ajili ya kupata eneo la ujenzi wa shule hiyo kama wamiliki wa shule hizo wataridhia Shule ijengwe Butiama.

Viongozi wengine waliokuwepo katika msafara huo ni Makamu Mwenyekiti wa taasisi ya ISHIK Foundation ambayo inamiliki shule za Feza na Mkurugenzi wa Mahusiano wa Shule za Feza Bwana Almas Mukanov.  

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa