• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mkuu wa Mkoa awataka wananchi kuchangamkia fursa za REA

Posted on: December 3rd, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Evans Alfred Mtambi leo ameongea na Waandishi wa Habari ofisini kwake kuhusiana na fursa tatu za nishati zinazotolewa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) zenye lengo la kuboresha maisha ya wananchi na hususan wanaoishi katika maeneo ya vijijini.  

Akizungumza katika tukio hilo, Mhe. Mtambi amezitaja fursa zinazotolewa na REA kuwa ni pamoja na uuzaji wa majiko ya gesi yenye ruzuku, uuzaji wa mifumo ya umeme jua yenye ruzuku na mikopo ya riba nafuu ya kuanzisha vituo vya mafuta vijijini.

“Wananchi watumie nafasi hii iliyotolewa na Serikali kujitokeza kwa wingi kuchangamkia fursa hizi zinazotolewa na REA ili kuweza kubadilisha maisha yao ikiwa ni pamoja na kuanzisha biashara za kuuza mafuta katika maeneo ya vijijini” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amesema katika fursa ya uuzaji wa majiko ya gesi yaliyowekewa ruzuku, REA itayatoa majiko kwenye mitungu ya gesi ya kilo sita kwa gharama ya shilingi 20,000/= tu kwa wananchi wa Mkoa wa Mara kuanzia mwezi januari, 2025.

Mhe. Mtambi amesema utoaji wa majiko hayo ni sehemu ya utekelezaji wa Mkakati wa Kitaifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia uliozinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan mwezi Mei, 2024 na utekelezaji wa jukumu la kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia hapa nchini ambalo wamepewa REA.

Mhe. Mtambi amesema fursa nyingine ni mikopo yenye riba nafuu ya kujenga vituo vya mafuta vijijini ambayo inatolewa kwa mtu mmoja mmoja au vikundi vya watu ambapo amewahamasisha wananchi kujiunga katika vikundi kuchangamkia fursa hiyo ya mikopo yenye riba nafuu.

Kanali Mtambi amesema fursa nyingine ni uuzaji wa mifumo ya umeme jua mahususi kwa ajili ya wananchi wanaoishi maeneo ya visiwani na maeneo ambayo hayajafikiwa na umeme kwa punguzo la asilimia hadi 75 ya bei za kawaida.

Mhe. Mtambi amesema fursa hizi zinatoa suluhisho la nishati safi ya kupikia, umeme wa gharama nafuu na mafuta na kuwahamasisha wananchi kuchangamkia fursa hizo zinazotolewa na Serikali.

Kwa Upande wake, Mhandisi Deusdedit Malulu kutoka Wakala wa Umeme Vijijini REA amesema wakala hiyo inatarajiwa kugawa mitungi ya kilo sita ya gesi pamoja na vifaa vyake 452,000 yenye thamani ya shilingi bilioni 8.6 hapa nchini.

“katika mitungi hiyo, Mkoa wa Mara utapewa mitungi ya gesi 19,350 yenye thamani ya shilingi milioni 350 ambapo kila wilaya inatarajiwa kupatiwa mitungi 3,255” amesema Mhandisi Malulu.

Mhandisi Malulu amesema wananchi watauziwa mitungi hiyo kwa gharama ya shilingi 20,000 na ili kuweza kununua mwananchi atatakiwa kuwa na namba au kitambulisho cha utaifa (NIDA) na kila mtu ataruhusiwa kununua jiko mmoja tu.

Mhandisi Malulu amesema REA inayo pia fursa ya wananchi kuuziwa mfumo wa umeme wa jua na vifaa vyake kwa punguzo la hadi asilimia 75 ya bei ya vifaa hivyo madukani ili kusogeza umeme wa uhakika na wa bei nafuu kwa wananchi wanaoishi mbali na umeme wa kawaida na hususan visiwani.

Mhandisi Malulu amesema REA pia inatoa mikopo ya hadi shilingi milioni 135 kwa mtu mmoja mmoja au vikundi kwa ajili ya uanzishwaji wa vituo vya mafuta vijijini kwa riba ya asilimia tano tu huku marejesho yanafanyika hadi miaka saba.

“Huu mkopo ni muafaka kwa watu wanaotaka kuanzisha biashara za mafuta katika maeneo ya vijijini na unalenga kupunguza ajali majumbani kwa wananchi wanaouza mafuta bila kufuata taratibu za uhifadhi wake” amesema Mhandisi Malulu.   

Kikao hicho kimehudhuriwa pia na Mhandisi wa TANESCO Mkoa wa Mara Mhandisi Nurdin Babu,  baadhi ya maafisa kutoka REA makao makuu, maafisa kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na Waandishi wa Habari wa vyombo mbalimbali vya habari.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa