• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mkuu wa Mkoa akutana na watu wenye ulemavu

Posted on: June 15th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi leo amekutana na watu wenye ulemavu wa Mkoa wa Mara katika ukumbi wa Chuo cha Utatibu Musoma na kupokea baadhi ya changamoto zinazowakabili watu wenye ulemavu katika Mkoa wa Mara.

Akizungumza katika kikao hicho, Mheshimiwa Hapi amewataka Maafisa Ustawi wa Jamii kuwasaidia watu wenye ulemavu ikiwa ni pamoja na kuwaombea ufadhili kwa wadau ;na kuwasaidia kuomba mikopo ya Halmashauri na kuifuatilia mikopo hiyo kwa niaba ya watu wenye ulemavu.

“Ninataka Maafisa Ustawi wa Jamii wa Halmashauri muwajibike katika kuwasaidia watu wenye ulemavu, kuwaombea ufadhili katika masuala mbalimbali kwa wafadhili na kufuatilia mikopo yao wanayoomba Halmashauri” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa kazi ya Afisa Ustawi wa Jamii ni pamoja na kuhakikisha kuwa watu wenye ulemavu masuala yao yanapewa kipaumbele na Halmashauri zao na wanasikilizwa wanapokuwa na shida katika ofisi za Halmashauri.

Wakati huo huo, Mkuu wa Mkoa amewaagiza Wakuu wa Wilaya zote za Mkoa wa Mara kuzindua Kamati za watu wenye ulemavu katika ngazi za Wilaya, Kata, Vijiji na Mitaa  katika wilaya zao kwa mujibu wa miongozo ya Serikali.

Mheshimiwa Hapi amemtaka Mkuu wa Chuo cha Maendeleo ya Jamii Buhare kukarabati ofisi na vyoo vinavyotumiwa na Shirikisho la Watu Wenye Ulemavu Mkoa wa Mara wakati anapofanya ukarabati majengo ya chuo hicho.

Mkuu wa Mkoa ameagiza Waganga Wakuu wa Halmashauri kuhakikisha dawa zote zinazotumiwa na watu wenye ulemavu wa akili na matatizo ya kisaikolojia zinapatikana wakati wote ili kuwaondolea changamoto za ukosefu wa dawa hizo wanazodai kuzipata.  

Amewataka wazazi wa Watoto wenye ulemavu kuwapeleka Watoto hao shule ili waweze kupata elimu itakayowasaidia kuweza kuyamudu maisha yao ya baadaye.

Aidha Mkuu wa Mkoa ameahidi kuwasaidia kupata ufumbuzi wa changamoto mbalimbali zinazowakabili watu wenye ulemavu katika Mkoa wa Mara zilizopo ndani ya mamlaka yake.

Mheshimiwa Hapi amechukua fursa hiyo kuwahamasisha watu wenye ulemavu kushiriki katika Sensa ya Watu na Makazi itakayofanyika hapa nchini tarehe 23 Agosti, 2022.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Shirikisho wa Watu Wenye Ulemavu Mkoa wa Mara Bwana Iddi Hamis Mtani amemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa kukutana na watu wenye ulemavu kwa mara ya pili baada ya kula nao futari wakati wa Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

Akisoma risala ya watu wenye ulemavu ameeleza kuwa wanakabiliana na changamoto mbalimbali ikiwemo ughali wa vifaa saidizi vinavyotumiwa na walemavu, ukosefu wa takwimu sahihi za watu wenye ulemavu, taasisi za fedha kukataa kutoa mikopo kwa walemavu waioona kutokana na kukosa utaalamu wa kuandika na kusoma maandishi ya nukta nundu na uchakavu wa majengo na miundombinu ya Kituo cha Watu wenye Ulemavu Nyabange.

Bwana Mtani amezitaja changamoto nyingine kuwa ni baadhi ya walemavu kutokunufaika na TASAF, halmashauri kutokutenga bajeti za kutosha kuhudumia watu wenye ulemavu na milolongo mirefu ya kupata mikopo ya Walemavu inayotolewa na Halmashauri.

Katika risala hiyo, Shirikisho la Watu Wenye Ulemavu wamemuomba Mkuu wa Mkoa kuwasaidia kupata kiwanja ambacho wamepatiwa na Manispaa ya Musoma ambacho wameshindwa kukilipia gharama za kulipa fidia inayokadiriwa shilingi 21,200,000/=

Mkoa wa Mara kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi unajumla ya watu wenye ulemavu mbalimbali 13,650 ikiwa ni miungoni mwa mikoa yenye watu wengi wenye ulemavu.

 Kikao cha Mkuu wa Mkoa na watu wenye ulemavu kimehudhuriwa na Afisa Usalama wa Mkoa, Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa, Mwakilishi wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, viongozi wa taasisi zinazotoa huduma katika Mkoa wa Mara na baadhi ya watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa