• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mkoa wa Mara wajipanga kuongeza uzalishaji wa Kahawa

Posted on: March 11th, 2020

Mkoa wa Mara umeanza kutekeleza kwa vitendo mkakati wake wa kuongeza uzalishaji wa zao la Kahawa kutoka tani 1,500 mwaka 2019 hadi tani 15,000 ndani ya miaka minne ijayo.

Hayo yameelezwa leo na Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kighoma Malima wakati wa hafla ya kupokea miche ya kahawa 40,000 iliyotolewa na Bodi ya Kahawa nchini (TCB) kwa ajili ya kupandwa katika mashamba mbalimbali kati ya miche 100,000 ambayo bodi hiyo iliahidi kuitoa katika Mkoa wa Mara.

“Sisi tunataka tuwe mfano katika kilimo bora cha kahawa hapa nchini, tumeanza na tunazidi kuendelea. Mpango wetu ni kupanda miche angalau milioni mbili kila mwaka katika Mkoa mzima” alisema Malima.

Amesema kwa sasa Mkoa wa Mara unalima kiasi kidogo cha kahawa aina ya Arabika katika wilaya za Tarime, Rorya na Butiama lakini imekuwa na ubora mkubwa na kufanikiwa kuongoza kwa ubora Afrika.

“Kama wakulima wetu watapata usimamizi mzuri wa mashamba yao, miche hii ya kahawa itawakomboa kwa kuwa inatoa mavuno mara kumi zaidi ya ile ya zamani ”alisema Mheshimiwa Malima.  

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Kahawa hapa nchini Prof. Jamal Katundu ameeleza kuwa Tanzania inampango wa kuongeza uzalishaji wa zao la kahawa kutoka tani 50,000 kwa hivi sasa hadi tani 200,000 ndani ya kipindi cha miaka mitano ijayo.

“Katika kutekeleza adhma hii, mwaka huu tunampango kwa kushirikiana na halmashauri za wilaya kupanda mashamba mawili makubwa ya mfano katika kila wilaya inayolima kahawa ambayo yatatumika kama mashamba darasa kwa wananchi wanaoyazunguka mashamba hayo”.

Ameushukuru Mkoa wa Mara kwa utayari wao katika kuongeza uzalishaji katika zao la kahawa ameahidi kuleta miche zaidi kama mikoa mingine iliyotengewa miche haitaonyesha utayari wa kuipanda miche hiyo.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu Mheshimiwa Anthony Peter Mavunde amesema kuwa kwa sasa serikali inatilia zaidi mkazo kwa vijana kujiajiri na kilimo ni fursa kubwa sana ya vijana kuweza kujiajiri kiurahisi.

Ameupongeza Mkoa wa Mara na Bodi ya Kahawa kwa jitihada za kuongeza uzalishaji wa zao la Kahawa hapa nchini. Aidha ametoa rai kwa mikoa yote hapa nchini kutenga maeneo ya kilimo kwa ajili ya vijana watakaohitaji kulima katika vikundi.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa