• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mkoa wa Mara wadhamiria kuboresha Elimu

Posted on: February 25th, 2020

Mkoa wa Mara umedhamiria kuboresha elimu ya Msingi na Sekondari mkoani humu kwa vitendo kwa kuboresha mazingira ya kujifunzia na ufundishaji na kuvunja kabisa mtandao wa wizi wa mtihani uliokuwepo miaka ya nyuma.

Akizungumza kwenye Kongamano la Wadau wa Elimu wa Mkoa wa Mara lililofanyika tarehe 23 Februari 2020, Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Malima amesema tumejitahidi sana kuboresha miundombinu ya shule za msingi na sekondari.

Akizungumzia kuhusu mtandao wa wizi wa mitihani mkoani Mara, Mheshimiwa Malima alisema “Mkoa wa Mara ulikuwa ni kitovu cha wizi wa mitihani hapa nchini, lakini tumefanikiwa kuuvunja mtandao wa wizi wa mitihani na sasa tunachokipata ndio hali halisi”. Amesema japokuwa awali Mkoa ulionyesha unafaulisha sana, lakini baadaye waligundua ufaulu huo ulitokana na wizi wa mtihani.

Mheshimiwa Malima amesema, wizi huu wa mitihani ungeachwa uendelee ungejenga kizazi cha watu wengi sana ambao hawajui chochote lakini wanavyeti vizuri.  “Ingekuwa ni hatari kwa maendeleo ya taifa letu kwa siku za baadaye”. Amesema katika mtandao huo kulikuwa na uhusika wa wadau karibu wote wa elimu na hususan wazazi ambao walikuwa wanatoa fedha za kununua mitihani.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa mdahalo huo na Mbunge wa Musoma Vijijini  Prof. Sospeter Muhongo alisema zamani Mkoa wa Mara ulikuwa na shule mbili tu za sekondari za umma Mara Sekondari na Musoma Alliance lakini zilikuwa zinafanya vizuri sana na wengi waliohitimu hapo walifaulu na kufanya vizuri sehemu nyingine walizoenda kusoma.

“Enzi zetu sekondari za binafsi zilizokuwepo chache lakini zilikuwa hazitushindi kabisa tuliokuwa tunasoma shule za serikali katika mashindano ya kitaaluma, zilitushinda katika mambo mengine”. Alisema Mhe. Muhongo. Alisema sababu kubwa zilizochangia wao kufanya vizuri ilikuwa ni ubora wa walimu waliokuwa wanawafundisha na mazingira mazuri ya kusomea katika maeneo ya shule yaliyokuwepo wakati huo.

Kongamano hilo lililofanyika katika Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Songe, lilihudhuriwa pia na wazazi, wanafunzi wa shule za msingi na sekondari, walimu, maafisa elimu wa ngazi za kata, halmashauri na ngazi ya mkoa. Aidha walihudhuria vyama mbalimbali ikiwemo Chama cha Walimu, Vyama vya Wakuu wa Shule, Vyama vya walimu wakuu, wanasiasa, watu maarufu na wananchi wakawaida.

Kongamano lilifanikiwa kutoa maazimio tisa ambayo ni pamoja na halmshauri ziandae mikakati ya kuboresha miundombinu ya elimu shuleni; mwanafunzi ambaye hataonekana shuleni kwa siku saba mfulilizo atalazimika kufika shuleni na mzazi wake na utaratibu wa utoaji chakula kwa wanafunzi shuleni ni lazima hivyo wazazi ambao hawatachangia chakula watachukuliwa hatua za kisheria.

Pia kongamano lilikubaliana kuwa walimu watoro wafikishwe kwenye mamlaka ya nidhamu na maamuzi yatolewe haraka ili kuimarisha uwajibikaji wa walimu; mahusiano kati ya walimu na jamii yaimarishwe ili kuboresha ufundishaji na ujifunzaji; vitendo vya mimba kwa wanafunzi na ukatili kwa watoto wa kike vitengenezewe mkakati wa kuvitokomeza na uwepo wa mpango bora wa kuishirikisha jamii kwenye maendeleo ya shule.

Aidha kongamali liliazimia kuwa serikali za vijiji ziwe na mkakati wa kuhakikisha usalama wa walimu kwenye mazingira yao na kongamano lingine la kutathmini maazimio ya kongamano hili lifanyike tarehe 30 Agosti, 2020.  

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa