• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mhe. Mtanda ataka maboresho utekelezaji wa Mkataba wa Lishe

Posted on: July 24th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Said Mohamed Mtanda leo ameongoza Kikao cha Tathmini ya Mkataba wa Lishe katika Mkoa wa Mara na kuwataka viongozi, watendaji na wataalamu kufanya maboresho katika utekelezaji wa Mkataba wa Lishe katika Mkoa wa Mara.

Akizungumza wakati wa kikao hicho, Mhe. Mtanda amewataka Maafisa Lishe wa Halmashauri kutekeleza kikamilifu majukumu yao ili kuwasaidia  Wakurugenzi, Wakuu wa Wilaya na watendaji wengine katika utekelezaji wa Mkataba wa Lishe.

“Ninyi mkitekeleza majukumu yenu vizuri, mtawakumbusha viongozi wenu na kuwapa tahadhari mapema wakati wa utekelezaji ili kuzitoa Halmashauri katika utekelezaji hafifu wa mkataba huu muhimu kwa ustawi wa jamii”amesema Mhe. Mtanda.

Mhe. Mtanda pia amewataka Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri kusimamia utekelezaji wa mkataba wa lishe hadi ngazi za vijiji, mitaa na kata na tarafa ili kuweza kuwafikia wananchi katika maeneo hayo.

Aidha, Mhe. Mtanda ameziagiza Halmashauri kuhakikisha vituo vyote vya kutolea huduma za afya vinakuwa na ubao wa kupimia urefu ili kuviwezesha vituo hivyo kupima hali za afya za wananchi wanaopata huduma za matibabu katika vituo hivyo.

Kwa upande wake, Katibu Tawala Mkoa wa Mara Bwana Msalika Robert Makungu ameeleza kuwa Mkataba wa Lishe katika baadhi ya Halmashauri hautekelezwi vizuri kwa sababu fedha za masuala ya lishe zinatengwa katika vyanzo ambavyo havina uhakika.

“Halmashauri nyingi zinatenga fedha za kutekeleza mkataba wa lishe kutoka katika mapato ya ndani au fedha za wafadhili vyanzo ambavyo havina uhakika sana na hivyo kusababisha utekelezaji hafifu wa Mkataba wa Lishe” amesema Bwana Makungu.

Bwana Makungu ameeleza kuwa kwa mujibu wa maelekezo ya Serikali, fedha zilizotengwa kwa ajili ya utekelezaji wa Mkataba wa Lishe zisipotolewa katika mwaka wa fedha husika zinapaswa kuwa deni katika mwaka wa fedha unaofuata ili kutekeleza shughuli zilizokuwa zimepangwa.

Kwa upande wake, Afisa Lishe kutoka Sehemu ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe Bwana Benson Sanga ameeleza kuwa Halmashauri ziangalie uwezekano wa kutenga fedha za kuwawezesha Wahudumu wa Afya Ngazi ya Jamii ili kuwawezesha kutoa elimu kuhusu masuala ya lishe kwa wananchi.

“Wahudumu wa Afya ngazi ya Jamii wakiwezeshwa wanaweza kupita nyumba kwa nyumba na kutoa elimu kwa mtu mmoja mmoja ambayo mtu ataisikiliza zaidi kuliko njia za mikutano ya hadhara inayotumika sasa ni njia ngumu kuweza kuwabadilisha wananchi” amesema Bwana Sanga.

Bwana Sanga ametoa mfano wa Halmashauri ya Chunya ambayo Wahudumu wa Afya Ngazi ya Jamii wametengenezewa vitambulisho, wamewapatiwa tisheti na kuwanunulia baskeli kwa awamu ili kuwawezesha kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

“Huu ni mfano mzuri wa kuigwa ambapo pamoja na kusaidia kuwawezesha wahudumu hawa, pia umewafanya watambulike kiurahisi katika jamii na kuwajengea kujiamini wanapotekeleza majukumu yao yakiwemo masuala ya lishe” amesema Bwana Sanga.

 Kikao cha tathmini ya Mkataba wa Lishe kimehudhuliwa na Wakuu wa Wilaya, Wakuu wa Sehemu na Vitengo wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, Wakurugenzi wa Halmashauri, Waganga Wakuu wa Halmashauri, Maafisa Lishe, Waweka Hazina, Maafisa Utumishi na Maafisa Mipango wa Halmashauri zote tisa za Mkoa wa Mara.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa