• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara yazungumza na viongozi wa Dini

Posted on: April 17th, 2020

16 Aprili 2020

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kighoma Ali Malima leo amefanya mazungumzo na viongozi wa madhehebu na jumuiya mbalimbali za kidini wanaofanya shughuli zao katika Mkoa wa Mara.

Akizungumza wakati wa kikao na viongozi hao Mkuu wa Mkoa ameeleza kuwa Tanzania na ulimwengu wote tupo katika mapambano makubwa dhidi ya janga la homa ya mapafu inayosababishwa na  virusi vya Corona maarufu kama COVID 19.

“Leo tumewaita hapa kutokana na umuhimu wenu katika masuala ya kiimani mnayoyaongoza katika jamii inayowazunguka” alisema Malima.

Alieleza kuwa pamoja na mambo mengine viongozi wa Mkoa wa Mara wanatarajia viongozi wa dini pamoja na kuliombea taifa, wasaidie katika juhudi za kupambana na ugonjwa wa Corona hapa nchini na hususan kwa wananchi wanaowahudumia.

“Ninawashukuru sana viongozi wote wa dini kwa maombi yenu ya kuliombea taifa hili mnayoendelea nayo, tunaendelea kumwomba Mungu atusikie kilio chetu” alisema Mheshimiwa Malima.

Akizungumza katika mkutano huu, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mara Dkt. Florian Tinuga ameeleza kuwa viongozi wa dini wanatakiwa kuendelea kupata elimu sahihi ya corona na kuisambaza kwa waumini wao ili kuwakinga na janga la corona.

Dkt. Tinuga amewataka viongozi hao kubuni njia mbalimbali za kuwaelimisha waumini ikiwa ni pamoja na nyimbo na kuonyesha mifano ya namna ya kujikinga na corona.

“Itakuwa vizuri kama kwenye kila ibada au swala, waumini wakapata nafasi hata ya dakika 10 kuambiwa habari za janga la Corona na namna ya kujikinga.

Kwa upande wake Askofu Michael Msoganzila wa Jimbo Katoliki Musoma alieleza kuwa kutokana na janga hili kanisa hilo limebadilisha sana namna ya kuendesha misa na kupunguza baadhi ya vitu ambavyo sio vya lazima.

Aidha Kanisa limetunga sala ambayo husaliwa katika kila familia kuliombea taifa na waumini wote na kumuomba Mungu aliepushe taifa katika janga la Corona.

“Hata hivyo kuna taasisi za elimu ambazo zinamilikiwa na taasisi ya dini ambazo kutokana na athari ya majanga ya corona itakuwa ngumu kuwalipa wafanyakazi wao mishahara hususan kama janga hili litaendele kwa muda mrefu” alisema Mloganzila

Kwa upande wake Shehe Mkuu wa Mkoa wa Mara Bwana Sheikh Msabaha Kassimu ameeleza kuwa anashukuru kuwa serikali imeruhusu masuala ya dini yaendelee wakati huu, na wao wanachukua tahadhari zote za kujikinga na corona.

 Katika mkutano huo Mkuu wa Mkoa aliambatana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Mara, maafisa waandamizi na wataalamu mbalimbali wa afya.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa