• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara yazindua utoaji wa chanjo ya HPV

Posted on: April 23rd, 2024

Katibu Tawala wa Wilaya ya Musoma Bwana Ally. S. Mwendo leo amemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Mara katika uzinduzi wa zoezi la utoaji wa chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi kwa mabinti wenye umri wa miaka 9-14 kimkoa iliyofanyika katika Shule ya Msingi Mkendo.

Akizungumza katika uzinduzi wa zoezi hilo, Bwana Mwendo amewatakaa wazazi na walezi kuhakikisha watoto wao wakike wanapata chanjo hiyo kwani ni salama na inatolewa bure katika  shule za msingi na sekondari na vituo vya kutolea huduma za afya.

“Chanjo hii inatolewa katika kampeni hii ya siku tano za wiki ya chanjo duniani, ni ile ile inayotolewa wakati wote na inatolewa bure, haina madhara na nimuhimu sana kwa mabinti ili kujikinga dhidi ya saratani ya mlango wa kizazi hapa nchini” amesema Bwana Mwendo.

Ameitaja kauli mbiu ya zoezi hilo kuwa ni Jamii inayochanjwa, Jamii yenye afya na kuwataka wananchi kuachana na imani potofu na taarifa zisizo rasmi na badala yake wawasikilize suhauri wa wataalamu wa sekta ya afya.

Kwa upande wake, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii Dkt. Zabron Masatu ameeleza kuwa Tanzania kupitia Wizara ya Afya na Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wameandaa chanjo ya saratani ya kizazi kwa wasichana wenye umri wa miaka 9-14.

Dkt. Masatu ameeleza kuwa utoaji wa chanjo hiyo katika Mkoa wa Mara umeanza tarehe 22-26 Aprili, 2024 kuanzia saa 1.30 asubuhi hadi saa 10 jioni katika shule za msingi, sekondari na katika vituo vya kutolea huduma za afya.

Kwa mujibu wa Dkt. Masatu jumla ya wasichana 229,249  wenye umri wa miaka 9-14 wanategemewa kupatiwa chanjo hiyo katika Halmashauri zote tisa za Mkoa wa Mara.

Uzinduzi wa zoezi la chanjo umehudhuriwa na Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Musoma, Wasimamizi wa Afya, Maafisa Elimu na watumishi wengine ngazi ya Mkoa na Manispaa ya Musoma.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa