• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara yazindua chanjo ya UVIKO 19

Posted on: August 6th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi leo tarehe 5 Agosti, 2021 amezindua utoaji chanjo ya UVIKO 19 kwa wananchi wa Mkoa wa Mara katika viwanja vya ofisi ya Mkuu wa Mkoa.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa utoaji wa Chanjo Mheshimiwa Hapi amewataka wananchi kuondoa hofu, chanjo ni salama na wataalamu wa afya wamethibitisha hilo.

“Chanjo hizi ni salama na niwaombe wananchi tutumie fursa hii adhimu ambayo serikali ya awamu ya sita imeitoa kupata chanjo ili iweze kutukinga na UVIKO 19” alisema Mheshimiwa Hapi.

Aidha amempongeza Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutumia diplomasia na kujenga hoja kufanikisha upatikanaji wa dozi milioni moja za awali ambazo serikali inazitoa bure kwa wananchi wake.

“Mheshimiwa Rais kwa mapenzi yake kwa watanzania ametutafutia chanjo hizi na sasa tunazipata bure na kuonyesha usalama wa chanjo hizi na yeye mwenyewe amechanjwa na anaendelea na jitihada za kutafuta chanjo nyingine” ameeleza Mheshimiwa Hapi.

Hata hivyo amewataka wataalamu wa afya kuendelea kutoa elimu kuhusu chanjo hiyo kwa wananchi ili waweze kuchanja kwa hiari yao wenyewe.

“Ndugu zangu ugonjwa upo, na katika Mkoa wa Mara tunawagonjwa na wengine tumewapoteza, na hapa tunapakana nan chi za Kenya na Uganda zote zina wagonjwa, kwa hiyo ninawasihi tuchanjwe na kuendelea kuchukua tahadhari za kujikinga” amesema Mheshimiwa Hapi. 

Kwa upande wake Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Albert Gabriel Msovela ameeleza kuwa kuwa kwa sasa Mkoa umepokea dozi 25,000 za chanjo na umetenga vituo 22 vya kutolea huduma ya chanjo kwa wananchi.

“Vituo hivi vinaweza kuongezwa kama kutaonekana kuna mahitaji ya kuongeza vituo zaidi ya hivi vya sasa ili wananchi wetu wapate chanjo kwa hiari na bila usumbufu” alisema Msovela.

Amewashukuru wananchi kwa mwitikio wao katika tukio la uzinduzi wa chanjo hiyo na kuwasihi watakaochanjwa kuendelea kuwashawishi wenzao wachanjwe.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mara Dkt. Juma Mfanga ameeleza kuwa chanjo iliyopo kwa sasa ni aina ya Johnson inayotengenezwa na kampuni ya Johnson and Johnson na mtu anachomwa mara moja tu hairudii.

“Chanjo hii ya UVIKO 19 ni salama na imefanyiwa utafiti na wataalamu wa ndani na nje ya nchi na kuthibitishwa na mamlaka zetu kuwa ni salama kwa matumizi na zinatolewa kwa kutumia utaratibu wa kawaida wa chanjo” alisema Dkt. Mfanga

Dkt. Mfanga ameeleza kuwa katika suala la chanjo kuna hofu kuu mbili, moja ni hofu ya ubora na ufanisi wa chanjo na pili ni hofu hofu ya kuchoma sindano “niwatoe hofu kwa kuwa sindano hii ya chanjo haiumi sana na chanjo ni bora na inafanyakazi vizuri” alisema Dkt. Mfanga.

Aidha amewataka watu kutulia kidogo mara baada ya kuchomwa chanjo ya UVIKO 19 na kama mtu atapata maudhi yoyote baada ya chanjo ni hali ya kawaida kwachanjo yoyote arudi katika kituo alipopatiwa chanjo atapatiwa huduma.

Aidha amewataka wananchi kuendelea kuchukua tahadhari na kufanya mazoezi ya viungo ili kukabiliana na maambukizi ya UVIKO 19 hata baada ya kupatiwa chanjo.  

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa