• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara yatangaza wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka 2021

Posted on: December 18th, 2020

Mkoa wa Mara leo tarehe 18 Desemba 2020 umetangaza matokeo ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza kwa mwaka 2021.

Akitangaza matokeo hayo, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bibi Karolina A. Mthapula amesema kati ya wanafunzi 51,822 waliofanya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi mwaka huu, wanafunzi 40,426 wamefaulu ambayo ni sawa na asilimia 77.98.

“Kati ya wanafunzi wote waliofaulu mtihani huo, wavulana ni 20,950 na wasichana ni 19,476 wakati kuna wanafunzi 11,396 ambao walifanya mtihani huo lakini hawakufaulu” alisema Bibi Mthapula.

Kwa mujibu wa Bibi Mthapula, kati ya wanafunzi wote waliofaulu, wanafunzi 7,804 wamekosa nafasi za kuchaguliwa awamu ya kwanza kutokana na uhaba wa vyumba vya madarasa ambapo mpaka sasa bado Mkoa unahitaji vyumba 156 ili watoto wote waliofaulu waweze kuanza shule.

“Naziagiza halmashauri kuhakikisha kuwa inakamilisha vyumba hivyo kabla ya tarehe 30 Januari 2030 ili wanafunzi wote waliofaulu waweze kujiunga na kidato cha kwanza” alisema Bibi Mthapula.

Hata hivyo alizipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Tarime na Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti kwa kuwa na vyumba vya madarasa vinavyokidhi mahitaji na ziada na kuzitaka halmashauri nyingine za mkoa huo kuiga mfano huo.

“Niwaombe wadau wenye uwezo kutuchangia kupitia halmashauri zetu ili kuweza kukamilisha kazi hii ya ujenzi wa madarasa ili watoto wetu waanze kusoma mapema iwezekanavyo” alisema Mama Mthapula.

Aidha aliwaambia wajumbe wa kikao hicho kuwa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Mara ikiongozwa na Mkuu wa Mkoa Mheshimiwa Adam Kighoma Ali Malima watafanya ukaguzi wa utekelezaji wa maagizo ya Waziri Mkuu kuanzia kesho tarehe 19 Desemba 2020 katika halmashauri zote za Mkoa huo.

Kwa upande wake Kaimu Afisa Elimu wa Mkoa wa Mara Bwana Freedence B. Serapion ameeleza kuwa zoezi la usajili wa wanafunzi limefanyika kupitia mtandao ambapo kwa ngazi ya kitaifa matokeo yametangazwa tarehe 17 Desemba 2020 na waziri mwenye dhamana.

“Wanafunzi hawa walianza darasa la kwanza mwaka 2014 wakiwa 62,596 na waliosajiriwa kufanya mtihani wa mwisho ni 51,882 wakati wengine 1,361 hawakufanya mtihani kutokana na sababu mbalimbali” alisema Bwana Serapion.

Aidha Bwana Serapion ameeleza kuwa ufaulu wa wanafunzi kwa ngazi ya Mkoa umepanda kwa asilimia 8.24 huku Wilaya ya Serengeti ikiongoza kwa kufanya vizuri zaidi kuliko wilaya nyingine za Mkoa wa Mara katika matokeo ya mtihani huo.

Aidha katika uchaguzi wa ngazi ya taifa wanafunzi 169 wamepangiwa shule za kitaifa ikiwemo wanafunzi wenye mahitaji maalum.

Kikao hicha cha uchaguzi wa wanafunzi kilihudhuriwa na wadau mbalimbali wa elimu wakiwemo wabunge, madiwani, Meya wa Manispaa ya Musoma, Wakuu wa Wilaya na watendaji wa halmashauri na Mkoa.

Mitihani ya Darasa la Saba kwa mwaka 2020 ilifanyika tarehe 7 na 8 Oktoba na matokeo ya mtihani huo yalitangazwa rasmi tarehe 23 Novemba 2020 na Baraza la Taifa Mitihani (NECTA)

Katika matokeo ya mwaka huu ufaulu wa wanafunzi umeongezeka na Mkoa umeshika nafasi ya 19 kutoka nafasi ya 26 kwa mwaka 2019.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa