• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara yapokea walimu 50 kutoka Zanzibar

Posted on: September 13th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mungiya Mzee leo amewapokea walimu zaidi ya 50 kutoka Chama cha Walimu Zanzibar walio katika ziara ya mafunzo na utalii katika Mkoa wa Mara.

Akizungumza na walimu hao, Mheshimiwa Mzee amewapongeza walimu hao kwa kufanya utalii wa ndani na kuchagua kuutembelea Mkoa wa Mara wenye vivutio vingi vya utalii na kihistoria ya Taifa letu. 

“Mara ni sehemu ambayo ina vivutio vingi vya asili ikiwemo Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, Makumbusho ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na kuongeza kuwa Mara ndio chimbuko la Tanzania” alisema Mheshimiwa Mzee.

Mheshimiwa Mzee ameeleza kuwa kwa niaba ya wananchi wa Mkoa wa Mara amefurahi sana kuona walimu hao wamekuja kufanya utalii na kujifunza katika Mkoa wa Mara na kuwataka warudi Mara watakapojisikia uchovu na msongo wa mawazo.  

Kwa upande wake, Katibu wa Chama cha Walimu Mkoa wa Mara ambaye ni mwenyeji wa walimu hao Bibi Suzan Shesha amemshukuru Mkuu wa Mkoa wa Mara kwa kuweza kuonana na walimu hao pamoja na ratiba za shughuli zake kuwa nyingi.

“Sisi pamoja na wageni wetu tunashukuru sana kwa kupata nafasi ya kuweza kukutana na walimu hawa, na tunakuahidi tutawatembeza maeneo yote watakayotaka kwenda na kuwapa ushirikiano wakati wote wakiwa katika Mkoa wa Mara” alisema Bibi Shesha.  

Kwa upande wake, Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Walimu Zanzibar (ZATU) Bwana Musa Abdi Hamis ameeleza kuwa ziara yao pamoja na kujifunza kutoka katika shule mbalimbali za Mkoa wa Mara, watatembelea vivutio vya utalii na nyumbani kwa Baba wa Taifa ili kuunga mkono jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuhamasisha utalii kupitia filamu ya Royal Tour.

Bwana Hamis ameeleza kuwa katika ziara hiyo, watatembelea shule mbalimbali za msingi, shule za sekondari zinazofanya vizuri sana na zile ambazo hazifanyi vizuri katika mitihani ya Taifa ili kuweza kujifunza.

Aidha, walimu hao wanatarajia kutembelea Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, maonyesho ya Mara International Expo yanayoendelea katika viwanja vya Mukendo, Manispaa ya Musoma, mpaka wa Tanzania na Kenya uliopo eneo la Sirari wilayani Tarime, Shule ya Msingi Mkendo aliyosoma Baba wa Taifa na nyumbani kwa Baba wa Taifa.

Walimu hao pia walitoa zawadi za viungo vya Zanzibar mbalimbali kwa Mkuu wa Mkoa na Chama cha Walimu Mkoa wa Mara.  

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa