• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara yapokea miradi ya zaidi ya milioni 200

Posted on: January 13th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mzee leo amepokea nyumba ya walimu, mradi wa maji na ufadhili wa wanafunzi wenye jumla ya thamani ya shilingi 222,500,000 kutoka Shirika la Zawadi Project.

Akizungumza katika hafla ya kupokea msaada huo, Mheshimiwa Mzee amelipongeza shirika hilo kwa msaada huo ambao unaisaidia jamii katika shule mbalimbali za  Serikali katika kata saba za Tarafa ya Chamriho, Wilaya ya Bunda.

Miradi iliyopokelewa ni nyumba ya walimu yenye uwezo wa kuchukua familia sita yenye thamani ya shilingi 120,500,000/=, mradi wa kisima, matenki na mtandao wa maji wenye thamani ya shilingi 49,000,000/= na ufadhili wa wanafunzi 256 wa shule za msingi na sekondari wenye thamani ya shilingi 53,000,000/=

Akiwa katika eneo hilo, Mheshimiwa Mzee amezindua mradi wa maji katika Shule ya Msingi Kambarage na nyumba ya walimu katika Shule ya Msingi Sarawe zilizojengwa kwa nguvu ya wananchi na ufadhili wa shirika la Zawadi Project.  

Mheshimiwa Mzee amemtaka Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Kambarage kubuni namna ya kukifanya mradi wa maji waliopewa na Shirika la Zawadi kuwa endelevu na kuweza kuleta manufaa yaliyotarajiwa.

Awali, Mratibu Mkazi wa Shirika la Zawadi Project Bwana Nelson Mafie ameeleza kuwa Shirika hilo linafanya miradi yenye lengo la kutoa ufadhili kwa wanafunzi wanaotoka katika mazingira magumu, kuboresha mazingira ya shule na kutoa mafunzo ya walimu kazini.

Kwa mujibu wa Bwana Mafie, miradi iliyopokelewa leo ni mwendelezo wa miradi mbalimbali ambayo shirika hilo limekuwa likiitekeleza katika kata mbalimbali za Tarafa ya Chamriho, Wilaya ya Bunda.

Bwana Mafie ameeleza kuwa ufadhili wa wanafunzi ni kuanzia shule ya msingi hadi vyuo vikuu kwa wanafunzi wanaofanya vizuri katika masomo yao.

Kwa mujibu wa Bwana Mafie ameeleza kuwa kwa sasa shirika linawafadhili jumla ya wanafunzi 256 ambapo kati yao wanafunzi 141 wapo shule za msingi, 115 wapo shule za sekondari 14 wapo Kidato cha Tano na Sita, 12 wapo katika mafunzi ya ufundi, 4 wapo vyuo vya kati na 7 wapo katika vyuo vikuu mbalimbali hapa nchini.

 Bwana Mafie ameeleza kuwa shirika hilo lenye makao yake makuu katika Mkoa wa Arusha, Katika Mkoa wa Mara Shirika hilo linafanya shughuli zake katika Wilaya ya Bunda Tarafa moja ya Chamriho.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa