• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara yajipanga kurahisisha watalii kuingia Serengeti

Posted on: November 5th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi leo tarehe 22 Oktoba 2021 amezungumzia namna Mkoa wa Mara unavyojipanga katika kuwarahisishia watalii wa ndani na nje ya nchi kuingia katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.

Mheshimiwa Hapi ametoa pongezi hizo wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kuzungumzia ushindi wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti kama hifadhi bora ya Afrika kwa mwaka wa tatu mfulilizo. 

“Serikali kwa sasa inaendelea kuupanua Uwanja wa Ndege wa Musoma ili ndege za abiria ziweze kutua, aidha mchakato wa ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Mugumu unaendelea ili ndege nyingine ziweze kutua katika uwanja huo” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa lengo la kuimarisha viwanja vya ndege nje ya hifadhi ni kwa ajili ya kupunguza ndege zinazotua hifadhini aidha kuruhusu ndege za abiria kuweza kutua karibu kabisa na hifadhi ili kuwavutia watalii wa kipato cha kati na cha chini kutoka ndani na nje ya nchi.  

Aidha Mheshimiwa Hapi amezungumzia pia barabara za kuingia katika Wilaya ya Serengeti zinaendelea kujengwa kwa kiwango cha lami na hivi vyote vikikamilika itawarahisishia watalii kuingia na kutoka Serengeti.

“Tunafahamu kuwa sio watalii wote ni matajiri, ndio maana serikali inataka kurahisisha usafiri wa kuingia katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ili kuvutia watalii wengi zaidi hususan wanafunzi, wastaafu na watu wenye uwezo wa kawaida” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa kutokana na uwekezaji huo wa serikali, wananchi wa Mkoa wa Mara wanatarajiwa kufaidika aaidi na fursa zitokanazo na utalii katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti kuliko ilivyo kwa hivi sasa ambapo watalii wengi wanapitia katika mikoa ya Mwanza na Arusha.

Aidha Mheshimiwa Hapi ameipongeza Hoteli ya Four Seasons Safari Lodge ambayo pia imepata ushindi katika tuzo hizo kama hoteli bora.

“Sisi kama Mkoa tunayo agenda kubwa ya kuendelea kuvitangaza vivutio vya utalii lakini pia kuifanya Tanzania na Dunia ijue kuwa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ambayo ni moja katika urithi mkubwa wa dunia ipo katika Mkoa wa Mara” alisema Mheshimiwa Hapi. 

Mheshiwa Hapi amempongeza pia Rais Samia Suluhu Hassan kwa jitihada zake za kutangaza utalii wa Tanzania na pamoja na mkakati wake wa kitaifa wa kuhakikisha tunakuwa na filamu itakayoitangaza Tanzania kimataifa umeanza kuzaa matunda.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa