• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara yajipanga kuongeza wanufaika wa CHF

Posted on: July 30th, 2021

Mkoa wa Mara umejipanga kuongeza idadi ya watu wanaonufaika na Mfuko wa  Bima ya Afya ya Jamii (CHF iliyoboreshwa) katika kupata matibabu katika vituo vya kutolea huduma.

Hayo yameelezwa leo tarehe 29 Julai 2021 katika kikao kazi cha wadau wa CHF iliyoboreshwa kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara iliyopo katika Manispaa ya Musoma.

Wakizungumza katika kikao hicho, wajumbe wa kikao hicho wamesema kuna tatizo katika kuhamasisha watu wajiunge na CHF iliyoboreshwa kutokana na sababu mbalimbali ambazo pia zinawakwamisha waliojiunga kuendelea kulipia kupitia mfumo huo wa matibabu.

Maazimio ya kikao hicho ni pamoja na kuboresha huduma katika vituo vya kutolea huduma za afya, kufunga mifumo ya malipo ya serikali (GOTHOMIS) katika vituo vyote vya kutolea huduma za afya na kuendelea kutoa elimu kwa wananchi ili waweze kuona faida ya kutumia CHF iliyoboreshwa.

“Katika kutoa elimu tutawashirikisha viongozi wa kisiasa na serikali na kutumia mifumo ya kuwafikia wananchi kupitia viongozi wao wa serikali za vijiji na mitaa ili waweze kutoa elimu sahihi kwa wananchi” walisema wajumbe hao

Maazimio mengine ni kuanzisha madawati ya CHF iliyoboreshwa katika vituo vya kutolea huduma za afya ili kutoa elimu kwa wananchi; kuongeza ushirikiano na maafisa wa sekta nyingine ngazi ya Mkoa wenye watu hadi kwenye vijiji na kata ili waweze kusaidia kutoa elimu.

Akizungumza katika kikao hicho Mratibu wa CHF Mkoa wa Mara Bi. Elizabeth Mahinya ameeleza kuwa kwa sasa Mkoa unawatu waliojiunga  na CHF iliyoboreshwa 11,192 hata hivyo kati yao watu 3,861 kadi zao zimeisha muda wake wa matumizi na hawajalipia tena ili kuendelea kuzitumia.

“Kwa sasa kumekuwa na tatizo la mwitikio mdogo wa wananchi kujiunga na waliojiunga muda wa matumizi ukiisha hawalipii tena ili waendelee kuwepo katika mfumo huu” alisema Bi. Mahinya.

Bibi Mahinya amesema kuwa kufuatia tatizo hilo Mkoa ulichukua hatua mbalimbali ambazo kwa sasa zimeanza kuzaa matunda na kuongeza idadi ya watu wanaojiunga na mfuko huo.

Ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Butiama ambayo awali ilikuwa chini katika uandikishaji lakini baada ya kuwakumbusha uandikishaji umepanda na wananchi wananufaika na CHF iliyoboreshwa.

Kwa upande wake Afisa wa Taasisi ya Health Promotion and System Strengthening (HPSS) katika Mikoa ya Simiyu, Shinyanga na Mara, Bwana Andrea Wilson Katamiti ameeleza kuwa CHF iliyoboreshwa inaweza kuwasaidia sana wananchi katika kupata huduma za afya kwa gharama nafuu.

“Familia yenye watu sita inalipia shilingi 30,000 na inatibiwa kwa kipindi cha mwaka mmzima katika vituo mbalimbali vya kutolea huduma za afya” ameeleza Bwana Katamiti.

Bwana Katamiti ameeleza kuwa vituo vya kutolea huduma za afya vinahitaji elimu zaidi ili viweze kuona kuwa vikiboresha huduma na kuvutia wanachama wengi wa CHF iliyoboreshwa vinaweza kupata fedha nyingi.

 CHF kama Mfuko wa Afya ya Jamii ni mpango wa hiari wa uchangiaji wa huduma za matibabu kwa ajili ya familia na kaya zenye kipato cha chini na zilizokwenye mfumo usiokuwa rasmi.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa