• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara yafikia asilimia 95.5 matumizi fedha za lishe

Posted on: August 21st, 2024

Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Mara Dkt. Khalfan Haule leo ameongoza kikao cha tathmini ya utekelezaji wa Mkataba wa Lishe katika Mkoa wa Mara kwa Mwaka 2023/2024 na kupongeza kwa mafanikio makubwa yaliyopatikana katika utekelezaji wa mkataba wa lishe.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi, Mhe. Haule amesema katika afua nyingi za lishe Mkoa wa Mara umepiga hatua kubwa ikiwemo ya utengaji wa fedha za utekelezaji wa mkataba wa lishe.

“Wakati tunaanza kutekeleza mwaka 2017/2018 Mkoa wa Mara ulikuwa unatumia chini ya asilimia 18 ya fedha zilizotengwa, lakini kwa mwaka huu uliopita Mkoa wa Mara umetumia kwa zaidi ya asilimia 95 ya fedha zilizotengwa kwa ajili ya utekelezaji wa Mkataba wa lishe” amesema Mhe. Haule.  

Mhe. Haule amezitaka Halmashauri kuongeza fedha inazotenga kwa ajili ya masuala ya lishe ili kuongeza utoaji wa huduma za lishe kwa walengwa na kupunguza changamoto ya utapiamlo na kuzitaka kutenga zaidi ya shilingi 1000 kwa kila mtoto.

Mkuu huyo wa Wilaya ya Musoma amezielekeza Halmashauri zilizopo mjini kama vile Mji wa Tarime, Manispaa ya Musoma na Halmashauri ya Mji wa Bunda ziongeze fedha zinazotengwa kutokana na kuhudumia watu wengi zaidi kuliko Halmashauri za Wilaya.

Mhe. Haule amewataka Wakurugenzi kuhakikisha Vitengo vya manunuzi vinaingiza kwenye mfumo wa manunuzi manunuzi yote yanayofanyika ili Halmashauri ziweze kupata taarifa sahihi za manunuzi kwenye mfumo kulingana na manunuzi yaliyofanyika na hususan katika afua za lishe.

Akitoa taarifa ya tathmini Kaimu Afisa Lishe Mkoa wa Mara Bi. Grace Martin Mgongolwa amesema katika kipindi hicho, matumizi ya fedha zilizotengwa kwa ajili ya lishe katika bajeti ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2023/2024 ni shilingi 758,966,854.86 ambapo kati yake shilingi 724, 545,126.77 zimetumika.

“Hii ni sawa na asilimia 95.5 ya fedha zote zilizopangwa kutumika kutekeleza afua za lishe katika Mkoa wa Mara ambapo hata hivyo baadhi ya fedha iliyotumika haikujazwa kwenye mfumo wa manunuzi na wataalamu wa manunuzi na hivyo kupunguza asilimia ya fedha zilizotumika” amesema Bi. Mgongolwa.

Bibi Mgongolwa ameyataja maneo ambayo bado yanachangamoto kuwa ni idadi ndogo ya wanafunzi wanaokula chakula shuleni, ukosefu wa mizani wa kupima uzito vijijini, ukosefu wa virutubishi vya kutimu watoto wenye utapiamlo wa kadri na upungufu wa chakula dawa cha kutibu watoto wenye utapiamlo mkali.

Bibi Mgongolwa amezitaka Halmashauri kuweka sheria ndogo zitakazohakikisha shule zote zinatoa chakula shuleni, kutenga fedha kwa ajili ya kununua vibao na mizani  wa kupima uzito katika vituo vya kutolea huduma za afya, kutenga fedha kwa ajili ya ununuzi wa chakula chenye virutubishi kwa ajili ya watoto wenye utapiamlo mkali na kuimarisha upatikanaji wa takwimu za udumavu.

Kikao hicho kimehudhuriwa na Wakuu wa Wilaya, Menejimenti ya Mkoa wa Mara, Meya na Wenyeviti wa Halmashauri, Makatibu Tawala wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri, baadhi ya wakuu wa Idara za Halmashauri na Timu ya uendeshaji wa shughuli za afya Mkoa wa Mara (RHMT).

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Mtambi aipongeza Bunda TC kwa hati safi miaka mitano mfululizo

    June 13, 2025
  • Mtambi aitaka Bunda DC kuwasilisha Mkakati wa kukusanya milioni 700

    June 13, 2025
  • Mtambi aipongeza Halmashauri ya Rorya

    June 12, 2025
  • Mtambi awataka wanawake kugombea nafasi za uongozi

    June 12, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa