• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara yadhamiria kuboresha barabara

Posted on: November 29th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi amewataka wakandarasi waliopewa zabuni za kujenga barabara mbalimbali katika Mkoa wa Mara kutimiza wajibu wao kikamilifu kwa mujibu wa mikataba yao.

Mheshimiwa Hapi ametoa kauli hiyo leo wakati akizungumza katika ufunguzi wa kikao cha Bodi ya Barabara ya Mkoa wa Mara kilichofanyika leo katika Ukumbi wa Uwekezaji uliomo katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

“Hatutakubali, hatutawavumilia wala hatutawafumbia macho wakandarasi wababaishaji ambao wanalipua kazi na kutokulipa wafanyakazi wao, wasiotekeleza kazi kwa haraka” alisema Mheshimiwa Hapi.  

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa wananchi wa Mkoa wa Mara walioko vijijini wanategemea sana barabara za TARURA na kutoa rai kuwa barabara zitakazofanyiwa kazi zilenge katika kuwasaidia wananchi kujenga uchumi wao na kuwaunganisha wananchi na huduma za kijamii.

Amezitaka Wakala wa Barabara nchini (TANROADS) na Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA) kutoa mafunzo kwa wakandarasi wa Mkoa wa Mara ili kuwajengea uwezo waweze kutekeleza miradi kwa wakati na ubora unaotakiwa.

Mheshimiwa Hapi amezitaka taasisi hizo wakati wa kutoa zabuni kwa wakandarasi kutoa kipaumbele kwa wakandarasi ambao wanauwezo, wasio na ubabaishaji katika kutekeleza miradi kwa mujibu wa mikataba yao.

“Hatutawapa kazi wakandarasi wa Mkoa wa Mara kwa kwa sababu tu ni wenzetu, tunawafahamu” alisema Mheshimiwa Hapi na kuwataka wakandarasi watekeleze miradi kwa viwango vinavyokubalika bila ubabaishaji.

Aidha amewataka Wakandarasi wote wanaotekeleza miradi mbalimbali katika Mkoa wa Mara kuaajiri watu kutoka katika maeneo wanapofanyia kazi hususan zile kazi ambazo hazihitaji ujuzi maalum ili kutoa ajira kwa wananchi wa Mkoa wa Mara

Mheshimiwa Hapi amewataka Wakuu wa Wilaya kusimamia miradi ya barabara inayotekelezwa katika maeneo yao na kuifuatilia kwa karibu kuweza kujiridhisha kuhusu hali halisi ya miradi hiyo.

Wakati huo huo, Kikao cha Bodi ya Barabara Mkoa wa Mara kimemchagua kwa kauli mmoja Mheshimiwa Jumanne Sagini, Mbunge wa Butiama, kuwa Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Barabara ya Mkoa wa Mara.

Mheshimiwa Sagini ambaye ni Katibu Mkuu na Katibu Tawala Mstaafu amechaguliwa baada ya Mkuu wa Mkoa wa Mara kupendekeza jina lake na wajumbe wa kikao hicho kuridhia kwa kauli mmoja.

Kikao hicho kimehudhuriwa na Wakuu wa Wilaya, Meya na wenyeviti wa halmashauri, wakurugenzi wa serikali za mitaa, Kamati ya Usalama ya Mkoa, wasimamizi wa masuala ya usafiri na Sekretarieti ya Mkoa na wadau wa usafiri katika Mkoa wa Mara.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa