• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara yaazimia kusimamia utekelezaji wa Afia za Lishe

Posted on: July 27th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri kusimamia utekelezaji wa afua za lishe katika halmashauri zao ili kuimarisha hali ya lishe katika Mkoa wa Mara.

Mheshimiwa Hapi ameeleza hayo leo tarehe 27 Julai 2021 katika kikao cha Kamati ya Afya ya Msingi (PHC) kilichofanyika katika ukumbi wa uwekezaji uliopo katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

“Ninataka utekelezaji wa afua za lishe upande angalau tuwe kwenye tatu bora kitaifa na sio tunakuwa namba 17 kama hali ilivyo kwa hivi sasa” alisema Mheshimiwa Hapi.

Amewasistiza wataalamu wa afya kuendelea kutoa elimu kwa wananchi ili waweze kuboresha mlo wao kulingana na mahitaji ya kiafya.

Ameeleza kuwa kwa taarifa alizonazo kwa takwimu za mwaka 2018 Mkoa wa Mara ulikuwa na udumavu kwa asilimia 29.2 kwa watoto.

“Udumavu kwa watoto wadogo ni janga la hatari sana ambalo huwezi kuliona kwa haraka ni sawa na bomu linalosubiri kulipuka kwa sababu unasababisha kuwa na watoto ambao hawawezi kufikiri vizuri, kusoma na kujifunza mambo kulingana na umri wao” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi amesema kuwa matibabu ya udumavu ni gharama kubwa sana kwa serikali na kuna maradhi mengi yanaayoambatana na lishe duni kwa watu wenye lika mbalimbali.

Mkuu wa Mkoa ameeleza kuwa kunapokuwa na udumavu kwenye jamii tunategeneza jamii ambayo haiwezi kuwa na tija katika uzalishaji, elimu, na nyanja nyinginezo.  

Amemtaka Katibu Tawala kuwaandikia barua wakurugenzi ambao halmashauri zao hazijafanya vizuri katika utekelezaji wa afua za lishe ili watoe maelezo ya kwa nini imetokea hivyo na ahadi yao ya kurekebisha hali hiyo.  

Akizungumza katika kikao hicho Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Albert Gabriel Msovela ameeleza kuwa Mkoa bado upo nyuma sana katika utekelezaji wa afua za afya na hivyo kunahaja ya watu wote kushirikiana ili kukabiliana na changamoto hiyo.

“Tathmini ya utekelezaji wa afua za lishe inaonyesha kuwa Mkoa wa Mara upo katika nafasi ya 17 kati ya mikoa 26 ya Tanzania Bara jambo ambalo haliridhishi kabisa” alisema Bwana Msovela.

Ameeleza kuwa hiyo inamaanisha watoto wengi wa Mkoa wa Mara wanao udumavu na hatua za haraka zisipochukuliwa hali hii itaendelea.

 “Mkoa unalima vyakula vya kutosha, tuna mifugo mingi na samaki pamoja na dagaa kutoka Ziwa Victoria, wananchi wanachohitaji ni elimu zaidi ili waweze kupanga mlo vizuri kulingana na mahitaji ya kiafya” alisema Msovela.

Bwana Msovela ameeleza kuwa changamoto kubwa aliyoiona katika masuala ya lishe ni utoaji wa taarifa, usimamizi na ufuatiliaji wa masuala ya lishe umekuwa mdogo.

Mwaka 2017 serikali iliingia mikataba na Wakuu wa Mikoa yote ili kuhakikisha suala la lishe linasimamiwa vizuri katika mamlaka za halmashauri za wilaya.

 Kikao cha Kamati ya Afya ya Msingi kimehudhuriwa na Wakuu wa Wilaya, Makatibu Tawala wa Wilaya, Wakuu wa vitengo vya Sekretarieti ya Mkoa, Wakurugenzi wa halmashauri, Waganga wakuu wa Wilaya, Maafisa Lishe na wataalamu wengine.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa