• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara Mshindi wa Kwanza Chanjo ya UVIKO 19 Kanda ya Ziwa

Posted on: November 5th, 2021

Mkoa wa Mara leo tarehe 5 Novemba 2021 umetambuliwa kwa mchango wake katika kuhamasisha na kuchanja wananchi chanjo ya UVIKO 19 na kumaliza chanjo kwa wakati na kufanikiwa kuwa  Mshindi wa Kwanza katika Mikoa yote ya Kanda ya Ziwa.

Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto imeutambua mchango huo na kutoa cheti cha utambuzi kwa kufanya vizuri katika awamu ya kwanza ya utoaji wa chanjo ya UVIKO iliyofanyika kuanzia tarehe 5 Agosti, 2021 hadi tarehe 2 Novemba 2021.

Utambuzi huo umetolewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Watoto, Prof. Abel N. Makubi katika ufunguzi wa kikao kazi cha Wakurugenzi wa Taasisi, Hospitali za Taifa, Maalum, Kanda, Rufaa za Mikoa Pamoja na Waganga Wakuu wa Mikoa kilichofanyika Jijini Dodoma.

Akizungumza wakati wa mawasilisho ya kikao hicho, Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mara Dkt. Juma Mfanga ameeleza kuwa mbinu mbalimbali zilitumika katika kufikia mafanikio hayo ikiwa ni pamoja na uchanjaji vituoni, huduma ya mkoba, huduma ya nyumba kwa nyumba, usimamizi shirikishi na ushirikishwaji wa viongozi.

“Katika kuhakikisha kila mtu mwenye umri wa miaka 18 na kuendelea anafikiwa na huduma hii ya chanjo, watoa huduma waliamua kutembelea nyumba moja baada ya nyingine kwenye maeneo mbalimbali ili kutoa elimu na chanjo kwa waliokuwa tayari kuchanjwa” alisema Dkt. Mfanga.

Dkt. Mfanga ameeleza kuwa awali, Mkoa wa Mara ulipokea chanjo za UVIKO 19 dozi 25,000 aina ya Janssen na uzinduzi wa chanjo hii kimkoa ulifanyika tarehe 5 Agosti 2021 na hadi kufika tarehe 4 Oktoba, 2021 chanjo zote zilitumika.

Ameeleza kuwa baadaye Mkoa wa Mara ulipokea chanjo nyingine dozi 9,850 kutoka Mkoa wa Mwanza ambazo zilisambazwa na kutumika kwa wananchi hadi tarehe 12 Oktoba 2021 zilimalizika.

Dkt. Mfanga ameeleza kuwa Mkoa wa Mara pia umepokea dozi 45,969 aina ya Sinopharm ambazo tayari zimeshasambazwa katika vituo vya kutolea huduma na kuanza kutolewa kwa wananchi.

“Hadi sasa wananchi waliochanjwa chanjo ya UVIKO 19 katika Mkoa wa Mara ni 32,479 ambayo ni sawa na asilimia 40 ya dozi 80,819 za chanjo ya UVIKO 19 zilizopokelewa katika Mkoa wa Mara” alisema Dkt. Mfanga.  

Awali, vituo 22 vilichaguliwa kutoa huduma ya chanjo ya UVIKO 19 katika Mkoa wa Mara, hata hivyo Mkoa uliongeza na kufika vituo 285 vya kutolea huduma za afya katika Halmashauri zote za Mkoa wa Mara.

Mikoa ya Kanda ya Ziwa inajumuisha mikoa ya Mara, Mwanza, Simiyu, Shinyanga, Geita, Tabora na Kagera. 

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa