• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara kutatua changamoto za Mgodi wa Barrick North Mara

Posted on: September 2nd, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mungiya Mzee leo amefanya ziara ya kutembelea  Mgodi wa Barrick North Mara uliopo katika eneo la Nyamongo, Wilaya ya Tarime na kuahidi kuzifanyia kazi changamoto mbalimbali zinazoukabili mgodi huo.

Akizungumza baada ya kupokea taarifa mbalimbali kuhusu utekelezaji wa shughuli za mgodi huo kutoka kwa viongozi wa mgodi wa Barrick North Mara wakiongozwa na Mkurugenzi Mkuu Bwana Apolinary Lyambiko, Mheshimiwa Mzee amesema baada ya kupokea taarifa na changamoto hizo wanajipanga kwa ajili ya kuzitatua.

“Mgodi unataka kupanua shughuli zake na upo tayari kulipa fidia, lakini kuna upinzani mkubwa wa kupata hayo maeneo, inafanyika tathmini lakini inaingiliwa na ujanja ujanja mwingi ambao unasababisha zoezi la kuendelea na uchimbaji likwame” ameeleza Mheshimiwa Mzee.

Mheshimiwa Mzee ameahidi kuyafanyia kazi maelekezo yote yaliyotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan alipotembelea Mkoa wa Mara Mwezi Februari, 2022 na Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuhusiana na maeneo yanayohitaji kulipwa fidia ili uchimbaji uendelee.

 “Tunaenda kujipanga tuone tunasaidia vipi kuweza kutatua changamoto hii kwa manufaa ya mgodi, wananchi wanaouzunguka mgodi na serikali ambayo ni mbia katika uwekezaji wa mgodi huu” alisema Mheshimiwa Mzee.

Aidha, Mheshimiwa Mzee amewashukuru viongozi wa mgodi huo kwa taarifa walizotoa ambazo zitasaidia katika kutatua baadhi ya changamoto zinazoukabili mgodi huo.

Awali wakitoa taarifa zao, viongozi wa Mgodi wa Barrick wameeleza kuwa changamoto nyingine ni wananchi ambao maeneo yao yamefanyiwa tathmini kukataa kuchukua fidia kwa madai kuwa fidia ni ndogo au wanataka wafanyiwe uthamini wa maeneo yao upya baada ya kufanya uwezekezaji zaidi baada ya tathmini ya awali.

Wamezitaja changamoto nyingine kuwa ni uvamizi wa mara kwa mara wa mgodi huo ambao wamedai kwa sasa tangia mwezi Aprili umepungua, lakini awali kulikuwa na wastani wa matukio ya uvamizi matano hadi saba kwa mwezi mmoja.

Wameeleza kuwa wavamizi huingia mgodini makundi makubwa ya watu 50- 70 hususan wakati wa mvua na huingia kulingana na koo zao na inapotokea mtu wa ukoo fulani ameiba madini wanaanza kunyang’anyana wao kwa wao na kujeruhiana lakini wakitoka wanaeleza kuwa wamejeruhiwa na askari wa mgodi.

Hata hivyo, pamoja na changamoto hizo viongozi hao wameeleza kuwa uzalishaji katika mgodi huo unaendelea vizuri na kwa mwaka huu kuna dalili kuwa mgodi ukavuka lengo lake katika uzalishaji.

Mkuu wa Mkoa aliambatana na Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Kamati ya Usalama ya Mkoa wa Mara, Kamishna Msaidizi wa Madini Mkoa wa Mara, Kamishna Msaidizi wa Ardhi Mkoa wa Mara na Mthamini wa Ardhi kutoka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi na kamati ya Usalama ya Wilaya ya Tarime.

Huu ni mwendelezo wa ziara za Mkuu wa Mkoa kujitambulisha baada ya kuteuliwa na Mheshimiwa Rais Julai 31 Mwaka huu na kuwasili Mkoa wa Mara Agosti 6, 2022 kuanza kazi.

 Kesho tarehe 3 Septemba, 2022 Mkuu wa Mkoa ataendelea na ziara yake ya kujitambulisha katika Wilaya ya Tarime.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa