• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara kufuatilia ukamilishaji wa Barabara ya Mika- Kilongwe

Posted on: May 31st, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Evans Alfred Mtambi leo amefanya ziara yake kwa kwanza katika Halmashauri ya Wilaya ya Rorya na kuahidi kuisadia wilaya ya Rorya kufuatilia ukamilishaji wa barabara ya Mika -Kilongwe yenye kilomita 57 inayojengwa kwa mita 200 hadi 400 kwa mwaka.

Akizungumza katika Ofisi za Chama cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Rorya Mhe. Mtambi ameeleza kuwa kutokana na umuhimu wa barabara hiyo kwa uchumi wa Wilaya ya Rorya na Mkoa wa Mara kwa ujumla ataifuatilia kuhakikisha inakamilishwa kwa haraka ili barabara hiyo iweze kukamilishwa kwa haraka.

“Nitaifuatilia barabara hii Wizarani ili kuhakikisha inapangiwa bajeti ya kutosha na mkandarasi analipwa kwa wakati ili barabara hii iweze kukamilika kwa wakati” amesema Mhe. Mtambi.

Akizungumzia barabara hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Rorya Mhe. Juma Chikoka ameeleza kuwa barabara hiyo ni muhimu sana kwa maendeleo ya kiuchumi ya Wilaya ya Rorya hivyo Wilaya inatamani ikamilishwe kwa haraka ili wananchi wapate huduma.

Mhe. Chikoka ameeleza kuwa tayari barabara hiyo imeshafanyiwa upembuzi yakinifu na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) hata hivyo imekuwa ikikamilishwa kwa vipande vidogo vidogo sana kila mwaka.

Akiwa katika ofisi za CCM, Mhe. Mtambi amepokelewa na kuzungumza na viongozi na watumishi wa CCM Wilaya ya Rorya wakiongozwa na Katibu wa CCM Wilaya ya Rorya Bwana Michael Bundala na viongozi wengine.

Baada ya mazungumzo na viongozi wa CCM, Mkuu wa Mkoa amekagua ujenzi wa barabara ya Mika- Kilongwe, ametembelea ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Rorya, amezungumza na watumishi wa Halmashauri ya Rorya katika Ukumbi wa Halmashauri na kukagua ujenzi wa hospitali ya Wilaya ya Rorya.

Baada ya hapo Mhe. Mtambi amekagua mradi wa ujenzi wa majengo ya Taasisi ya Utafiti wa Samaki (TAFIRI) katika eneo la Sota na kuhitimisha ziara yake kwa kufanya mkutano wa hadhara na wananchi wa Kata ya sota.

 Katika ziara hiyo, Mhe. Mtambi ameambatana na Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Rorya, viongozi wa CCM Wilaya ya Rorya, Mwenyekiti, Menejimenti na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya na watendaji wakuu wa taasisi za umma zilizopo katika wilaya hiyo.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa