• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Malima awataka Butiama kutenda haki

Posted on: June 6th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kighoma Ali Malima amewataka viongozi na watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Butiama kujitathmini na kuwatendea haki wananchi wa halmashauri hiyo.

Mheshimiwa Malima ametoa kauli hiyo leo tarehe 4 Juni 2020 wakati alipohudhuria baraza maalum la madiwani kwa ajili ya kujadili hoja mbalimbali zilizotolewa na Ofisi ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).

“Ninaomba wote tuliopo hapa leo tujitathmini, tunaitendea haki halmashauri hii na kama tunayoyafanya yanawanufaisha wananchi au yanaendana na dhamira ya serikali ya kuiendeleza halmashauri hii ambayo ipo nyumbani kwa Baba wa Taifa?” alisema Malima.

Aidha amewaasa madiwani na watendaji wa Halmashauri ya Butiama kushirikiana na kuondoa changamoto mbalimbali zilizokuwa zimejitokeza baina yao.

Mheshimiwa Malima ameeleza kuwa ameanza ziara yake katika Halmashauri ya Butiama kwa sababu madiwani na watendaji wa Halmashauri hawakuitendea haki halmashauri hiyo na kuiwezesha kupata hati yenye mashaka katika taarifa ya CAG ya mwaka wa fedha 2018/2019.

Kwa mujibu wa Mheshimiwa Malima, Halmashauri ya Wilaya ya Butiama ingeweza kupata mapato mengi ya ndani kama watendaji na madiwani na viongozi wengine wangeshirikiana na kuwa kitu kimoja.

Katika taarifa ya CAG, Halmashauri ya Wilaya ya Butiama ilikuwa na jumla ya hoja 72 ambapo kati yake hoja 41 ni za zamani kuanzia mwaka wa fedha 2013/2014 hadi 2017/2018 wakati hoja 31 ni kwa ajili ya mwaka wa fedha 2018/2019.

Hata hivyo baadhi ya hoja hizo za CAG zimefutwa baada ya CAG kuridhika na majibu yaliyotolewa na Halmashauri ya Wilaya ya Butiama na nyingine zipo katika hatua mbalimbali wa utekelezaji wake.

Wakizungumza katika kikao hicho madiwani walikiri kuwepo kwa changamoto kubwa za ushirikiano baina ya madiwani na watendaji hususan kwa baadhi ya wakurugenzi wa halmashauri hiyo waliookuwepo hapo awali. Hata hivyo wamempongeza Mkurugenzi wa sasa Bibi Diana Sound kwa kazi kubwa ambayo ameanza kuifanya katika halmashauri hiyo ikiwa ni pamoja na kurejesha vikao vya kawaida vya Baraza la Madiwani. 

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa