• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Malima amtaka DED Musoma DC kujenga Vichomea taka

Posted on: June 15th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kighoma Ali Malima amemtaka Mkurugenzi  Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma kujenga vichomea taka vinne kwa ajili ya vituo vya afya na zahanati za halmashauri hiyo hadi tarehe 30 Juni 2020.

Mheshimiwa Malima ametoa agizo hilo leo tarehe 8 Juni 2020 katika kikao maalum cha Baraza la Madiwani kwa ajili ya kujadili hoja za Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za serikali kwa mwaka wa fedha 2018/2019.

“Haiwezekani vituo vyote vya kutolea huduma za afya katika halmashauri hii kutokuwa na vichomea taka na mashimo ya kutupia kondo la nyuma, hali hii haikubaliki” alisema Mheshimiwa Malima.

Mheshimiwa amesema kwa kuwa ujenzi wa vichomea taka na mashimo haya vilikuwemo katika bajeti ya mwaka wa fedha 2019/2020 anamtaka Mkurugenzi kufanyakazi hiyo katika muda uliobakia na kuwasilisha taarifa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa.

Aidha amemtaka Mkurugenzi huyo kuwasimamia vizuri watendaji wake hususan katika kujibu hoja mbalimbali zinazotolewa na wakaguzi wa hesabu za serikali.

“Mimi nimesikitika sana kwa hoja hizi, ninavyoamini mimi huyu Mkurugenzi ni bora sana lakini watendaji wake mumemwangusha. Na hata ukiangalia hoja nyingi ni ndogondogo sana na zina majibu yake sasa sielewi kwa nini hazikuwasilishwa kwa mkaguzi wakati anakagua” alisema Mheshimiwa Malima.

Aidha Mkuu wa Mkoa wa Mara ameahidi kuandika barua kwa Wizara ya Fedha na Mipango kuhusu fedha za ujenzi wa Hospitali ya wilaya ambazo zilichukuliwa na Hazina baada ya mwaka wa fedha 2018/2019 kuisha zaidi shilingi milioni 500 ambazo bado zinahitajika kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa hospitali hiyo.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Musoma Dkt. Vicent Naano Anney ameipongeza halmashauri hiyo kwa ukusanyaji wa mapato na kwa mwaka wa fedha 2019/2020 wamefikia asilimia 97 ya lengo la makusanyo.

Aidha Dkt. Anney ameipongeza halmashauri hiyo kwa kuongeza mapato yanayotokana na uvuvi ambapo awali halmashauri ilikuwa inapata shilingi milioni 100 kwa mwaka wakati kwa mwaka huu 2019/2020 halmashauri imekusanya zaidi ya shilingi milioni 800.

 Katika ukaguzi wa Mwaka wa fedha 2018/2019 Halmashauri ya Wilaya ya Musoma ilipata hati safi na ilikuwa na jumla hoja 60 ambapo kati ya hizo hoja za nyuma 17 na hoja mpya za mwaka 2018/2019 ni 43.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Mtambi aipongeza Bunda TC kwa hati safi miaka mitano mfululizo

    June 13, 2025
  • Mtambi aitaka Bunda DC kuwasilisha Mkakati wa kukusanya milioni 700

    June 13, 2025
  • Mtambi aipongeza Halmashauri ya Rorya

    June 12, 2025
  • Mtambi awataka wanawake kugombea nafasi za uongozi

    June 12, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa