• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Majaliwa aagiza kukamatwa wawili Serengeti

Posted on: February 28th, 2024

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb.) leo amemuagiza Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara ACP Salum Morcase kuwakamata Mkuu wa Kitengo cha Fedha na Uhasibu wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti na Mfanyabiashara wa Serengeti aliyeshiriki katika wizi wa fedha za Serikali zaidi ya shilingi milioni 213.

Akizungumza katika kikao hicho, Mheshimiwa Majaliwa amewataja waliohusika na wizi wa fedha hizo kuwa ni pamoja na Bwana Saad Katunzi Shabailu Mwekahazina wa Halmashauri ya Serengeti na mfanyabiashara wa Mji wa Mugumu Bwana Daudi Matinde ambao baada ya kuhojiwa na timu kutoka ofisi ya Waziri Mkuu walikili kuhusika katika tukio hilo.

“Katika wizi huo, Mkurugenzi wa Halmashauri, Baraza la Madiwani, viongozi wa TAMISEMI hawakuwa na taarifa za wizi huo kwa sababu umefanywa katika mtandao unaowahusisha watumishi wa tatu wa TAMISEMI kutoka Kitengo cha Treasury Single Account (TSA)” amesema Mhe. Majaliwa.   

Mhe. Majaliwa ameeleza kuwa tarehe 10 Juni, 2023 walitumia mwanya wa kuiombea kibali fedha ya bakaa kwa barua iliyosainiwa na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo kwenda hazina, na ilipofika tarehe 30 Juni,2023 walikuwa wameshamaliza matumizi ya fedha iliyoombewa kibali.

Mhe. Majaliwa ameeleza kuwa baada ya kufanikiwa kutoa fedha hizo Bwana Ishabailu alipanda basi hadi kituo cha mabasi cha Nyegezi Jijini Mwanza na kukabidhi shilingi milioni 150 kwa Bwana Zabron Mponzi ambaye alisema fedha hizo zilikuwa zinahitajika haraka kwa wakubwa Dodoma nay eye akapewa shilingi milioni 39.

Mhe. Majaliwa amelitaka Baraza la Madiwani kuwa makini katika matumizi ya fedha za Serikali na kuwasimamia watumishi wa Serikali kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

Wakati huo huo, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mara limemkamata Bwana Shabailu wakati kikao cha Waziri Mkuu na watumishi pamoja na viongozi wa Wilaya ya Serengeti kikiwa kinaendelea kwa ajili ya kwenda kumfungulia mashtaka.

Akiwa Serengeti, Mhe. Majaliwa amefanya mkutano wa hadhara katika Uwanja wa Sokoine mjini Mugumu na kuelekea Wilaya ya Tarime ambapo amezungumza na wananchi wa Nyamwaga katika Halmashauri ya Wilaya ya Musoma.

 Baada ya Hapo Mhe. Waziri Mkuu kesho atafanya ziara katika Wilaya ya Rorya na kuhitimisha katika Wilaya ya Tarime ambapo atafanya mikutano katika eneo la Sirari na katika uwanja wa Serengeti Tarime Mjini.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa