• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Madaktari Bingwa wa Mama Samia watibu wagonjwa 2,244 Mara

Posted on: December 7th, 2024

Timu ya Madaktari Bingwa na Bobezi wa Mama Samia 42 walioweka kambi ya siku tano katika Hospitali ya Rufaa ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere (Kwangwa) wamefanikiwa kuwatibu wagongwa 2,244 huku wagonjwa 74 wakifanyiwa upasuaji na wagonjwa 46 wakipatiwa rufaa ya kupata matibabu zaidi katika Hospitali ya Rufaa ya Bungando.

Akizungumza katika halfa ya kuhitimisha kambi hiyo iliyofanyika katika Hoteli ya MK iliyopo Manispaa ya Musoma, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Gerald Musabila Kusaya amesema madaktari Bingwa madaktari hao wakiwa Mkoa wa Mara wamefanya kazi kubwa kwa manufaa ya maisha ya wananchi.

“Wananchi wa Mkoa wa Mara wanawashukuru sana na wangependa muendelee kutoa huduma hapa lakini wanafahamu huko mlipotoka pia wanawahitaji kwa ajili ya watu wengine kupata huduma” amesema Bwana Kusaya.

Bwana Kusaya amewakaribisha Madaktari Bingwa hao kama wanataka kuhamia au kuja kusaidia kutoa huduma za kibingwa katika hospitali hiyo au hospitali nyingine zilizopo katika Mkoa wa Mara na kuwaomba kama wanaushauri wa namna ya kuboresha huduma wautoe ili kuboresha utoaji wa huduma za afya katika Mkoa wa Mara.

Bwana Kusaya ambaye katika hafla hiyo alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi amewashukuru pia wataalamu wa afya wa Mkoa wa Mara walioshiriki kwa namna moja au nyingine katika utoaji wa huduma katika kambi hiyo na kuwataka kuendelea kuwahudumia wananchi kwa weledi.

Kwa upande wake, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii Dkt. Zabron Masatu amesema katika kambi hiyo, Hospitali ya kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere imefanikiwa kukusanya shilingi milioni 186 ambazo ni fedha taslimu na madai ya bima za afya zilizohusika katika kambi hiyo.

“Hospitali imetumia milioni 30 kwa ajili ya kulipa stahiki za watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere walioshiriki kwenye kambi hiyo pamoja na maandalizi ya kambi hiyo” amesema Dkt. Masatu   

Dkt. Masatu amewashukuru viongozi wa Mkoa wa Mara, Ofisi ya Rais TAMISEMI na Wizara ya Afya kwa kuandaa na kuratibu kambi maalum ya matibabu ambayo imesaidia katika kuwapatia matibabu ya kibingwa na bobezi wananchi wa Mkoa wa Mara.

Dkt. Masatu amezishukuru Hospitali zote za Mikoa ya Kanda ya Ziwa na Hospitali za Rufaa za Kanda za Chato na Bugando kwa kuwaruhusu na kuwawezesha Madaktari Bingwa na Bobezi walioshiriki katika kambi hiyo maalum ya siku tano.  

Akizungumza wakati wa kuwakaribisha viongozi katika hafla hiyo, Mganda Mfawidhi wa Hospitali ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Dkt. Osmund Dyegura amesema kambi maalum ya madaktari bingwa wa Mama Samia katika Hospitali za Rufaa za Mikoa ilianza mwaka 2022 katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu.

Dkt Dyegura amesema tayari Kambi kama hiyo mbali na Mkoa wa Simiyu pia imeshawahi kufanyika katika Mkoa wa Kagera na sasa Mkoa wa Mara na kote imekuwa ikileta manufaa makubwa kwa wananchi wanaopatiwa huduma.

Dkt. Dyegura amesema malengo ya kambi hiyo kusogeza huduma za kibingwa jirani na wananchi, kuwajengea uwezo wataalamu wa afya, kuibua wagonjwa ambao watapelekwa kupata matibabu zaidi katika Hospitali za Rufaa za Kanda.

Kambi ya Madaktari Bingwa na Bobezi wa Mama Samia imefanyika kuanzia tarehe 2-6 Desemba, 2024 na madaktari hao wakati wanawasili walipokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi tarehe 2 Desemba, 2024 katika Hospitali ya Rufaa ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kanali Mtambi ateta na viongozi wa NHIF

    August 05, 2025
  • Mtambi ataka maboresho utoaji wa mikopo ya asilimia 10

    August 06, 2025
  • Mtambi ataka Hamasa Mbio za Mwenge wa Uhuru

    August 06, 2025
  • Kilimo cha alizeti kinga dhidi ya uvamizi wa tembo- Mtambi

    August 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa